Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 48:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Kwa hiyo, siku zinakuja ambapo nitamupelekea wamimiaji ambao wataimimia divai yake. –Ni ujumbe wa Yawe.– Wataimwanga yote kutoka vyombo vyake na kuvivunja vipandevipande.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 48:12
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Utawaponda kwa fimbo ya chuma, utawavunja kama chungu cha mufinyanzi!’ ”


Kama ndege wanavyohangaika na kurukaruka, wakiwa wamefukuzwa kutoka chicha zao, ndivyo wabinti wa Moabu wanavyokuwa kwenye vivuko vya Arnoni.


Kuporomoka kwa ukuta huo, ni kama kupasuka kwa chungu ambacho kimepasuliwa vibaya sana, bila kubaki kigae cha kuopolea moto ndani ya jiko, au kuchotea maji katika kisima.


Wakubwa wake wanawatuma watumishi wao maji; watumishi wanakwenda kwenye visima, lakini hawapati maji; wanarudi na vyombo vitupu. Kwa ajili ya haya na mahangaiko wanaangalia chini.


Kisha wewe utavunja ule mutungi mbele ya watu wale watakaoenda pamoja nawe,


Muomboleze, enyi wachungaji; mulie na kugaagaa katika majivu, enyi wakubwa wa kundi. Siku za kuchinjwa kwenu na kusambazwa zinakaribia. Mutauawa kama kondoo dume wanene.


basi, nitayaita makabila yote ya kaskazini pamoja na mutumishi wangu Nebukadneza, mufalme wa Babeli. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nitawaleta waishambulie inchi hii na wakaaji wake pamoja na mataifa yote jirani. Nitawaangamiza kabisa, na kuwafanya kuwa kitu cha kuchukiza, cha kuzomewa na kuzarauliwa milele.


Moabu amestarehe tangu ujana wake, ametulia kama divai katika mutungi. Hajamimiliwa toka chombo kimoja katika chombo kingine, hajapata kupelekwa katika uhamisho. Kwa hiyo angali na onjo yake, harufu yake nzuri haijabadilika hata kidogo.


Halafu Wamoabu watapata haya kwa ajili ya mungu wao Kemosi, kama vile watu wa Israeli walivyopata haya kwa ajili ya kutegemea Beteli.


Mwangamizaji wa Moabu na miji yake anashambulia, vijana wake wazuri wamechinjwa. –Ni ujumbe wa Mufalme, jina lake Yawe wa majeshi.–


Juu ya nyumba za Moabu na katika viwanja vyao hakuna kinachosikilika lakini maombolezo tu. Mimi nimemuvunja Moabu kama chombo kisichotakiwa na mutu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Mwangamizaji atapita katika kila muji, hakuna muji utakaomwepuka; mabonde yataangamia, nafasi zenye kunyooka zitaharibiwa, kama vile Yawe alivyosema.


Mwangamizaji amekuja kukushambulia, ee Ninawe. Chunga kuta zako! Weka ulinzi katika barabara! Ujiweke tayari! Kusanya nguvu zako zote!


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ