Leo nimekupa mamlaka juu ya mataifa na falme, ukuwe na mamlaka ya kuongoa na kubomoa, mamlaka ya kuharibu na kuangamiza, mamlaka ya kujenga na ya kupanda mbegu.
Basi, huyo malaika aliyezungumuza nami akamwambia yule mwenzake: Kimbia umwambie yule kijana kwamba si lazima Yerusalema ukuwe na kuta, kama sivyo hapatakuwa nafasi ya kuwatoshelea wakaaji wake wengi na nyama watakaokuwa ndani yake.
Kama simba anavyotoka kwenye maficho yake, mwangamizaji wa mataifa ameanza kuja, anakuja kutoka pahali pake, kusudi aharibu inchi yenu. Miji yenu itabaki mabomoko matupu, bila kukaliwa na mutu yeyote.
Kutoka vilele vya mawe makubwa ninawaona, kutoka juu ya milima nawachungulia, hilo taifa linalokaa peke yake, lisilojiona kuwa sawa na mataifa mengine.
Atakapofika ataiangamiza inchi ya Misri. Kwa hiyo waliopangiwa kufa kwa ugonjwa watakufa kwa ugonjwa, waliopangiwa kukamatwa mateka, watakamatwa mateka; waliopangiwa kufa kwa vita watakufia katika vita.