Katika taabu zao zote, hakumutuma mujumbe mwingine kwa kuwasaidia, lakini yeye mwenyewe alikuja kuwaokoa; kwa upendo na huruma yake aliwakomboa. Aliwabeba na kuwakamata tangu zamani.
Haya ndiyo maneno nabii Yeremia aliyosema katika mwaka wa ine wa utawala wa Yoyakimu mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda na Baruku mwana wa Neria akayaandika katika kitabu:
Yeye anatufariji katika taabu yetu yote, kusudi tupate kuwafariji wale wanaokuwa katika taabu yoyote kwa kuwaletea faraja tuliyopokea kutoka kwa Mungu.
Kwa maana tuko na Kuhani Mukubwa asiyekosa kujua mwenyewe uzaifu wetu. Maana yeye alijaribiwa katika njia zote sawasawa na sisi, lakini hakufanya zambi.