Nilimupa Baruku mwana wa Neria mujukuu wa Masea ile barua ya ununuzi mbele ya binamu yangu Hanameli na washuhuda waliokuwa wametia sahihi juu ya barua ya ununuzi, na mbele ya Wayuda wote waliokuwa wameikaa katika baraza la walinzi.
Basi, Baruku alisoma maneno ya Yeremia kutoka katika kile kitabu mbele ya watu wote, ndani ya nyumba ya Yawe, katika chumba cha Gemaria mwana wa Safanu aliyekuwa katibu. Chumba hicho kilikuwa katika baraza la juu, kwenye mulango mupya wa nyumba ya Yawe.
Mufalme alimwamuru mwana wake Yerameli, Seraya mwana wa Azirieli na Selemia mwana wa Abudieli, wamukamate katibu Baruku na nabii Yeremia. Lakini Yawe aliwaficha.
Halafu Yeremia akamwita Baruku mwana wa Neria. Naye Baruku akaandika katika kitabu maneno yote yaliyotoka katika kinywa cha Yeremia sawa vile Yawe alivyokuwa amemwambia.
Wakubwa wakamwambia mufalme: Inafaa mutu huyu auawe kwa maana anawavunja moyo waaskari ambao wameachwa katika muji huu na watu wote kwa jumla, kwa kusema maneno kama hayo. Yeye hawatakii watu hawa mema lakini mabaya.
walikuwa wanawaogopa Wakaldea tangu wakati Isimaeli mwana wa Netania, alipomwua Gedalia mwana wa Ahikamu ambaye mufalme wa Babeli alikuwa amemusimika kuwa mutawala wa inchi.
wanaume, wanawake, watoto, wabinti wa mufalme na kila mutu ambaye Nebuzaradani mukubwa wa waaskari alikuwa amemwachia Gedalia mwana wa Ahikamu mujukuu wa Safanu. Wakamupeleka vilevile nabii Yeremia na Baruku mwana wa Neria.