tafazali, uwasikilize kutokea kule mbinguni, usamehe zambi za watumishi wako, watu wako Waisraeli, na uwafundishe kufuata njia nzuri. Kisha unyeshe mvua katika inchi yako hii ambayo uliwapa watu wako kwamba itakuwa mali yao.
Kisha, nikatoa maagizo kuwa sisi wote tufike karibu na muto Ahara kusudi tufunge kula chakula na kujinyenyekeza mbele ya Mungu wetu na kumwomba atulinde na kutuongoza katika safari yetu pamoja na watoto wetu.
watu wengi wataenda kule na kusema, Mukuje tupandie kwenye mulima wa Yawe, tuende kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo, apate kutufundisha njia zake, nasi tutafuata mapito yake. Maana sheria itakuja kutoka Sayuni; neno la Yawe kutoka Yerusalema.
Yawe anasema hivi: Musimame katika masanganjia, muangalie. Muulize juu ya matukio ya zamani. Mutafute pahali panapokuwa njia nzuri muifuate, nanyi mutaweza kupumzika. Lakini wao wakasema: Hatutafuata njia hiyo.
mataifa mengi yataufikia na kusema: Tuende juu kwenye mulima wa Yawe, tuende katika nyumba ya Mungu wa Yakobo, kusudi atufundishe njia zake, nasi tuzifuate. Maana sheria itatoka kule Sayuni; na neno la Yawe kule Yerusalema.
Heri wangekuwa siku zote na mawazo kama haya wakiniheshimu na kushika amri zangu! Mambo yao yote yangewaendekea vizuri, wao wenyewe na wazao wao milele.