Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 41:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Katika mwezi wa saba, Isimaeli mwana wa Netania, mujukuu wa Elisama, wa ukoo wa kifalme, mumoja wa wasimamizi wa mufalme alifika Misipa kwa Gedalia pamoja na watu kumi. Wakati walipokuwa wakikula chakula kule Misipa,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 41:1
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Abeneri aliporudi Hebroni, Yoabu alimupeleka pembeni kwenye mulango sawa vile anataka kuzungumuza naye kwa siri. Hapo Yoabu akamukata Abeneri katika tumbo kwa sababu Abeneri alikuwa amemwua ndugu yake Asaeli, na Abeneri akakufa.


Mara tu Atalia mama ya mufalme Ahazia alipoona kwamba mwana wake ameuawa, alitoka, akaangamiza watu wote wa jamaa ya kifalme.


Mufalme Nebukadneza wa Babeli akamuchagua Gedalia mwana wa Ahikamu, mujukuu wa Safanu, kuwa mutawala wa watu wote wa Yuda ambao hawakupelekwa Babeli.


Katika mwezi wa saba, Isimaeli mwana wa Netania, mujukuu wa Elisama, aliyekuwa wa ukoo wa kifalme, akafika kwa Gedalia pamoja na watu kumi, akamushambulia Gedalia, akamwua. Vilevile, akawaua Wayuda na Wababeli waliokuwa naye.


Lakini wakati Atalia mama ya Ahazia alipoona kwamba mwana wake ameuawa, alitoka akaangamiza jamii yote ya kifalme ya Yuda.


Wananilipa mabaya kwa mazuri yangu, na chuki kwa mapendo yangu.


Wanasema: “Magonjwa haya yatamwua; hatatoka tena ndani ya kitanda chake!”


Kiburi kinasababisha tu ugomvi, lakini kwa wanaokubali shauri jema kuna hekima.


Kasirani ni kali na hasira inaangamiza; lakini ni nani anayeweza kupingana na wivu?


alikwenda kwenye nyumba ya kifalme na kuingia katika chumba cha katibu. Mule mulikuwa wakubwa wote: katibu Elisama, Delaya mwana wa Semaya, Elnatana mwana wa Akibori, Gemaria mwana wa Safanu, Zedekia mwana wa Hanania, na wakubwa wote.


Wale wakubwa walipokwisha kuweka kitabu kile katika chumba cha Elisama katibu wa mufalme, walimwendea mufalme ndani ya kiwanja, wakamujulisha mambo yote.


Wakamutoa Yeremia kwa Gedalia mwana wa Ahikamu, mujukuu wa Safanu, amupeleke katika nyumba yake. Basi, Yeremia akaishi pamoja na wanainchi wengine.


Basi, Yohana mwana wa Karea pamoja na wakubwa wote wa waaskari kutoka katika pori, walifika kwa Gedalia, kule Misipa, wakamwambia:


Kama ukiamua kubaki, basi rudi kwa Gedalia mwana wa Ahikamu, mujukuu wa Safanu, ambaye mufalme wa Babeli amemusimika kuwa mutawala wa miji yote ya Yuda, ukae naye kati ya wanainchi wengine. Kama sivyo, kwenda kwenye unaona unastahili kwenda. Basi, mukubwa wa walinzi akamupa Yeremia vyakula na zawadi, kisha akamwacha ajiendee.


Kisha Yeremia akaenda Misipa kwa Gedalia mwana wa Ahikamu, akakaa naye pamoja na wanainchi waliobaki katika inchi.


Wakubwa wote wa waaskari kutoka katika pori pamoja na watu wao, waliposikia kwamba mufalme wa Babeli alikuwa amemusimika Gedalia mwana wa Ahikamu, kuwa mutawala wa inchi, na kwamba alikuwa amewaweka chini ya usimamizi wake wanaume, wanawake na watoto, ni kusema watu wakosefu kabisa katika inchi ambao hawakupelekwa katika uhamisho kule Babeli,


walimwendea Gedalia kule Misipa. Watu hao walikuwa Isimaeli mwana wa Netania, Yohana na Yonatani wana wa Karea, Seraya mwana wa Tanumeti, nao wana wa Efai kutoka muji Netofa, na Yezania wa muji wa Makati; wote pamoja na watu wao.


Kisha akachagua mutu mumoja wa jamaa ya kifalme, akafanya naye mapatano, akamwapisha kiapo cha uaminifu. Aliwaondoa wakubwa wengine katika inchi akawapeleka mbali


“Sisemi juu ya ninyi wote; ninawajua wale niliowachagua. Lakini inafaa maneno haya yanayosemwa na Maandiko Matakatifu yatimie: ‘Yule aliyechangia chakula nami, amenigeuka.’


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ