Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 40:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Wakubwa wote wa waaskari kutoka katika pori pamoja na watu wao, waliposikia kwamba mufalme wa Babeli alikuwa amemusimika Gedalia mwana wa Ahikamu, kuwa mutawala wa inchi, na kwamba alikuwa amewaweka chini ya usimamizi wake wanaume, wanawake na watoto, ni kusema watu wakosefu kabisa katika inchi ambao hawakupelekwa katika uhamisho kule Babeli,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 40:7
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini aliacha wamoja wa watu waliokuwa wamasikini kabisa katika inchi. Aliwaacha watunze mizabibu na kulima mashamba.


Basi, sehemu ya ukuta wa muji ukabomolewa, naye mufalme pamoja na waaskari wote wakakimbia wakati wa usiku wakipitia katika bustani ya mufalme kwenye mulango katikati ya kuta mbili, wakaenda upande wa Araba, ingawa Wababeli walikuwa wameuzunguka muji.


Nebuzaradani, mukubwa wa walinzi wa mufalme, aliwaacha katika inchi ya Yuda watu wamoja wamasikini ambao hawakukuwa na kitu chochote, akawagawanyia mashamba ya mizabibu na kuwapa maeneo ya kulima wakati huohuo.


Wakamutoa Yeremia kwa Gedalia mwana wa Ahikamu, mujukuu wa Safanu, amupeleke katika nyumba yake. Basi, Yeremia akaishi pamoja na wanainchi wengine.


Naye Zedekia, mufalme wa Yuda na waaskari wake wote walipowaona, walitoroka. Walitoka inje ya muji usiku, wakipitia katika bustani ya mufalme, kwenye mulango katikati ya kuta mbili, wakatelemukia kwenye bonde la muto Yordani.


Kisha, Nebuzaradani, mukubwa wa walinzi wa mufalme, aliwapeleka katika uhamisho kule Babeli watu waliokuwa wamebaki katika muji na wale waliokuwa wamejitoa kwake pamoja na wafundi wote waliokuwa wamebaki.


Katika mwezi wa saba, Isimaeli mwana wa Netania, mujukuu wa Elisama, wa ukoo wa kifalme, mumoja wa wasimamizi wa mufalme alifika Misipa kwa Gedalia pamoja na watu kumi. Wakati walipokuwa wakikula chakula kule Misipa,


Kisha, Isimaeli aliwakamata wabinti wa mufalme mateka na watu wote waliobaki kule Misipa, watu ambao Nebuzaradani, mukubwa wa walinzi, alikuwa amewaweka chini ya ulinzi wa Gedalia mwana wa Ahikamu. Isimaeli mwana wa Netania, aliwakamata mateka hao, akaondoka, akaenda kwa Waamoni.


Lakini Yohana mwana wa Karea, pamoja na wakubwa wote wa waaskari, waliposikia juu ya uovu ambao Isimaeli mwana wa Netania, alikuwa ameufanya,


wanaume, wanawake, watoto, wabinti wa mufalme na kila mutu ambaye Nebuzaradani mukubwa wa waaskari alikuwa amemwachia Gedalia mwana wa Ahikamu mujukuu wa Safanu. Wakamupeleka vilevile nabii Yeremia na Baruku mwana wa Neria.


Lakini Nebuzaradani mukubwa wa waaskari walinzi wa mufalme, aliwaacha watu wamoja waliokuwa wamasikini kabisa katika inchi, wakuwe watunza mizabibu na walimaji.


Watu wote wa inchi watamupatia mufalme wa Waisraeli sadaka hizo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ