Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 40:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Huu ni ujumbe uliotolewa kwa Yeremia kutoka kwa Yawe wakati Nebuzaradani mukubwa wa walinzi wa mufalme alipomuruhusu Yeremia aondoke Rama. Huyo mukubwa alimukamata Yeremia akifungwa minyororo, pamoja na wafungwa wengine wote wa Yerusalema na Yuda ambao walikuwa wamepelekwa katika uhamisho kule Babeli.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 40:1
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Katika mwaka wa makumi tatu na sita wa utawala wa mufalme Asa, Basha, mufalme wa Israeli, alishambulia inchi ya Yuda na kuanza kujenga muji wa Rama kusudi apate kuzuia mutu yeyote asitoke wala asiingie kwa Asa, mufalme wa Yuda.


Yeye anavunja na kufungua milango ya shaba, na kukatakata vifungio vya chuma.


Mungu anayekaa pahali pake patakatifu, ni Baba ya wayatima na mulinzi wa wajane.


Yawe anasema hivi: Sauti imesikilika katika muji wa Rama, maombolezo na kilio cha uchungu. Rakeli anawalilia watoto wake, wala hataki kufarijiwa kwa ajili yao, maana wote hawako tena.


Kisha, Nebuzaradani, mukubwa wa walinzi wa mufalme, aliwapeleka katika uhamisho kule Babeli watu waliokuwa wamebaki katika muji na wale waliokuwa wamejitoa kwake pamoja na wafundi wote waliokuwa wamebaki.


Nyuma ya siku kumi, neno la Yawe lilimufikia Yeremia.


Siku ya tano ya mwezi wa kumi, mwaka wa kumi na mbili tangu tulipopelekwa katika uhamisho, mutu mumoja aliyetoroka kutoka Yerusalema alikuja kwangu, akasema: Muji Yerusalema umetekwa!


Lakini Paulo akajibu: “Kwa sababu gani munalia na kunivunja moyo? Mimi niko tayari, si kwa kufungwa tu kule Yerusalema, lakini hata kufa vilevile kwa ajili ya jina la Bwana Yesu.”


Basi ni kwa sababu hii nimewaita kusudi tuonane na niseme nanyi, kwa maana ninafungwa na munyororo huu kwa ajili ya tumaini ambalo Waisraeli wanakuwa nalo.”


Mimi ni mujumbe wa Habari ile Njema, ijapokuwa sasa ninakuwa katika kifungo. Basi muniombee kusudi nipate kusema kwa uhodari, sawa inavyonipasa kusema.


Kisha, alikuwa akirudi Rama, maana kule ndiko kulikuwa kwake. Aliwaamulia Waisraeli haki zao kule, na kumujengea Yawe mazabahu kule.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ