Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 4:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Kwa hiyo, muvae gunia, muomboleze na kulia; kwa maana Yawe hajaondoa hasira yake kali kwenu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 4:8
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Alimwanga juu yao hasira yake kali, kasirani, chuki na taabu, na kuwashushia kundi la wamalaika waangamizaji.


Hakuna! Mutajikunja tu kati ya wafungwa na kuangamia pamoja na wanaouawa katika vita. Hata hivyo, hasira yake haijatulia, angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.


Mulie, maana siku ya Yawe imekaribia; inakuja kama uharibifu kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu.


Siku hiyo, Yawe wa majeshi alitaka mulie na kuomboleza, munyoe nywele na kuvaa nguo za gunia.


Mutetemeke kwa woga, enyi munaojiikalia tu; mutetemeke kwa hofu, enyi munaostarehe! Muvue nguo zenu, mubakie uchi, mujifungie nguo ya gunia katika viuno vyenu.


Kwa hiyo hasira ya Yawe iliwawakia watu wake, akaunyoosha mukono wake juu yao, akawaazibu. Milima ikatetemeka, maiti zao zikakuwa kama takataka katika barabara za muji. Hata hivyo, hasira yake haijatulia, angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.


Ingawa aliwaazibu watu, hawakumurudilia Yawe wa majeshi.


Uovu unawaka kama moto unaoteketeza michongoma na miiba; unawaka kama moto katika pori, na kutoa moshi muzito unaopanda juu katika anga.


Muomboleze, enyi wachungaji; mulie na kugaagaa katika majivu, enyi wakubwa wa kundi. Siku za kuchinjwa kwenu na kusambazwa zinakaribia. Mutauawa kama kondoo dume wanene.


Hasira ya Yawe haitatulia, mpaka atakapotimiza na kukamilisha mapenzi ya moyo wake. Kutakuja siku ambazo mutaelewa vema mambo hayo.


Moabu imepatishwa haya maana imevunjika. Muomboleze na kuililia. Mutangaze kandokando ya muto Arnoni, kwamba Moabu imeharibika kabisa.


Yawe anasema: Muvae magunia, enyi watu wangu na kugaagaa katika majivu. Muomboleze kwa uchungu, kama mutu anayemulilia mwana wake wa pekee, maana mwangamizaji atakuja, na kuwashambulia kwa rafla.


Enyi wapita njia wote, hivi hamujali kitu? Muangalie, muone kama kuna aliyepatwa na uchungu kama mimi, uchungu Yawe alioniletea siku ya hasira yake kali.


Wakikuuliza hivi: Kwa nini unaomboleza? Utawaambia: Ninaomboleza kwa sababu ya habari zinazokuja. Kila mutu atavunjika moyo, mikono yao yote itaregea; kila mutu anayeishi atazimia na magoti yao yataregea. Habari hizo zinakuja kweli, nazo zinatimia. –Ni Bwana wetu Yawe anayesema hivyo.


Wewe mwanadamu! Toa unabii useme hivi: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Muomboleze na kusema: Ole kwetu siku ile!


Enyi makuhani, muvae magunia kwa kuomboleza, mulie, enyi munaotumika kwenye mazabahu. Muingie katika hekalu muomboleze usiku kucha! Sadaka za chakula na kinywaji zimetoweka katika nyumba ya Mungu.


Nitazigeuza sikukuu zenu kuwa kilio, na nyimbo zenu za furaha kuwa maombolezo. Nitawavalisha ninyi wote magunia kwa huzuni na kunyoa vichwa vyenu upaa, kama kuomboleza kifo cha mutoto wa pekee. Na siku ya mwisho itakuwa ya uchungu mukubwa.


Enyi watu wa Yuda, munyoe vichwa vyenu kwa kuwaomboleza watoto wenu wapenzi; mupanue upaa wenu ukuwe mupana kama wa tai, maana watoto wenu watawaacha kwenda katika uhamisho.


Basi, Yawe akamwambia Musa: Utwae viongozi wote wa Israeli, uwatundike mbele yangu jua kati, kusudi kasirani yangu juu yenu ipite.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ