Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 4:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Kama simba anavyotoka kwenye maficho yake, mwangamizaji wa mataifa ameanza kuja, anakuja kutoka pahali pake, kusudi aharibu inchi yenu. Miji yenu itabaki mabomoko matupu, bila kukaliwa na mutu yeyote.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 4:7
33 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nebukadneza mufalme wa Babeli akaishambulia inchi ya Yuda. Yoyakimu akamutumikia kwa miaka mitatu halafu akaacha kumutii, akamwasi.


Katika siku ya kumi ya mwezi wa kumi, mwaka wa tisa wa utawala wa Zedekia, Nebukadneza mufalme wa Babeli akafika na waaskari wake kwa kushambulia Yerusalema. Akapiga kambi mbele ya muji ule na kujenga ngazi kuuzunguka.


Inchi yenu imeharibiwa kabisa; miji yenu imeteketezwa kwa moto. Wageni wamebeba mazao ya inchi yenu mbele ya macho yenu, imeharibiwa kama vile Sodoma.


Nimemusikia Yawe wa majeshi akisema hivi: Hakika nyumba nyingi zitabaki tupu, zile kubwa na nzuri zitabaki wazi bila wakaaji.


Mimi nikauliza: Bwana, mpaka wakati gani? Naye akanijibu: Mpaka wakati miji itakapobaki tupu bila wakaaji, nyumba bila watu, na inchi itakapoharibiwa kabisa.


Simba wananguruma kwa ajili yake, wananguruma kwa sauti kubwa. Wameiharibu kabisa inchi yake, miji yake imebaki mabomoko pasipo watu.


Yawe anasema hivi juu ya nyumba ya kifalme ya Yuda: Ingawa unaonekana vizuri kama inchi ya Gileadi, kama vichwa vya milima ya Lebanoni, ninaapa kwamba nitakufanya kuwa jangwa, ukuwe muji usiokaliwa na watu.


Nitawatayarisha waangamizaji wakufikie, kila mumoja akishika silaha yake. Watazikata nguzo zako nzuri za mierezi, na kuzitumbukiza katika moto.


Yawe amewaacha watu wake, kama vile simba anavyoacha pango lake; inchi yao imekuwa jangwa tupu, kwa sababu ya vita na hasira kali ya Yawe.


basi, nitayaita makabila yote ya kaskazini pamoja na mutumishi wangu Nebukadneza, mufalme wa Babeli. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nitawaleta waishambulie inchi hii na wakaaji wake pamoja na mataifa yote jirani. Nitawaangamiza kabisa, na kuwafanya kuwa kitu cha kuchukiza, cha kuzomewa na kuzarauliwa milele.


Kwa nini umetabiri kwa jina la Yawe, ukisema kwamba nyumba hii itaharibiwa kama ile ya Shilo na muji huu utakuwa ukiwa, bila wakaaji? Na watu wote wakamuzunguka Yeremia katika nyumba ya Yawe.


Lakini kama taifa lolote au utawala wowote hautajiweka chini ya mamlaka ya Nebukadneza mufalme wa Babeli, na kukataa kubeba katika shingo yao zile nira atakazowalazimisha kubeba, basi nitaliazibu taifa hilo kwa vita, njaa na magonjwa makali mpaka nitakapoliangamiza kabisa kwa njia yake. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Yawe anasema hivi: Katika muji huu ambao munasema kwamba umekuwa ukiwa bila watu wala nyama, katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalema ambazo ni tupu, bila watu wala nyama, humo kutasikilika tena sauti za vicheko, sauti za furaha,


Nitawaamuru nao wataurudia katika muji huu. Wataushambulia, watauteka na kuuteketeza kwa moto. Nitaifanya miji ya inchi ya Yuda kuwa ukiwa bila wakaaji. –Ni ujumbe wa Yawe.


Kelele la waaskari wapanda-farasi na la wapiga mishale litakaposikilika, watu wote watakimbia. Wamoja wao watakimbilia katika vichaka, wengine watajificha katikati ya mawe. Kila muji utaachwa tupu; hakuna mutu atakayekaa ndani yake.


Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli anasema hivi: Ninyi mumeona hasara yote niliyouletea Yerusalema na miji yote ya Yuda. Miji hii ni mabomoko mpaka leo wala hakuna mutu anayeishi humo.


Kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa mufalme, jina lake Yawe wa majeshi– kweli adui anakuja kuwashambulia: ni hakika kama vile Tabori unavyokuwa mulima, kama vile mulima Karmeli unavyoonekana kutoka katika bahari.


Kama vile simba anavyochomoka kutoka ndani ya vichaka vya muto Yordani na kuingia kwenye mbuga, ndivyo nitakavyowafukuza kwa rafla Waedomu toka katika inchi yao. Nami nitamuweka huko mutawala yeyote nitakayemuchagua. Maana, ni nani anayeweza kulinganishwa nami? Nani anayeweza kunishitaki? Ni muchungaji gani anayeweza kunipinga?


Kwa hiyo simba kutoka pori atawaua; imbwa wa pori kutoka jangwa atawararua. Chui anaivizia miji yao. Kila mutu anayetoka humo atararuliwa vipandevipande, kwa sababu zambi zao ni nyingi, maasi yao ni makubwa.


Israeli ni kama kondoo wanaowindwa na kufukuzwa na simba. Kwanza waliangamizwa na mufalme wa Asuria, na sasa Nebukadneza mufalme wa Babeli, amevunjavunja mifupa yake.


Kama vile simba anavyotoka ndani ya vichaka vya muto Yordani na kuingia kwenye mbuga, ndivyo nitakavyowafukuza kwa rafla watu wake kutoka kwake. Nami nitamuweka huko mutawala yeyote nitakayemuchagua. Maana, ni nani anayeweza kulinganishwa nami? Nani anayeweza kunishitaki? Ni muchungaji gani anayeweza kunipinga?


Kelele za farasi wa waadui zinasikilika tokea Dani, kwa mulio wa farasi wao wa vita, inchi nzima inatetemeka. Wanafika na kuharibu inchi na vyote vinavyokuwa ndani yake, kuangamiza muji pamoja na wote wanaokaa humo.


Nami nikauliza: Kuna mutu anayekuwa na hekima apate kueleza mambo haya? Ni nani aliyeongea na Yawe hata aweze kutangaza kwa nini inchi imeharibiwa na kufanywa tupu kama jangwa hata hakuna mutu anayepita humo?


Miji yenye watu itateketezwa, na inchi itakuwa ukiwa. Nanyi mutatambua kwamba mimi ni Yawe.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: tosha kitambulisho chako cha kifalme na taji yako, maana mambo hayatabaki kama yalivyokuwa. Wanaokuwa chini watanyanyuliwa, wanaokuwa juu watashushwa!


Wewe mwanadamu! Imba wimbo wa kuomboleza juu ya Mufalme wa Misri. Wewe Mufalme wa Misri unajiona kuwa simba kati ya mataifa, lakini wewe ni kama mamba tu katika maji: unachomoka kwa nguvu kwenye mito yako, unayavuruga maji kwa miguu yako, na kuichafua mito.


Kwa sababu ya ukubwa aliomupa, watu wa makabila yote, mataifa yote na luga zote walitetemeka na kumwogopa. Nebukadneza aliweza kumwua mutu yeyote aliyetaka na kumwacha muzima mutu yeyote aliyetaka. Aliyetaka kumupandisha cheo alimupandisha, aliyetaka kumushusha cheo alimushusha.


Nyama wa kwanza alikuwa kama simba, na alikuwa na mabawa kama ya tai. Nikiwa ninamwangalia, mabawa yake yaliongolewa, naye akainuliwa na kusimama kwa miguu miwili kama mutu. Kisha, akapewa akili ya kimutu.


Miji yenu nitaiteketeza, pahali penu patakatifu nitapafanya jangwa na harufu zenu nzuri za sadaka sitazikubali.


Nitawatawanya ninyi kati ya watu wa mataifa na kuchomoa upanga juu yenu. Inchi yenu itakuwa ni ukiwa na miji yenu uharibifu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ