Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 4:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Muinue bendera ya vita kuelekea Sayuni, kusudi mukimbie, wala musisitesite! Yawe analeta hasara, analeta maangamizi makubwa kutoka kaskazini.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 4:6
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Enyi wakaaji wa Yerusalema, mutoke, mutoke inje ya muji, muwatayarishie njia watu wenu wanaorudia! Mujenge! Mujenge barabara na kuondoa mawe yote! Muweke bendera kuwa kitambulisho kwa ajili ya watu.


Musikilize ile fujo! Angalia inakuja. Kunatokea shindo kubwa upande wa kaskazini. Taifa kutoka kaskazini linakuja kuifanya miji ya Yuda kuwa jangwa, wataigeuza mapango ya mbweha!


Basi Sasa, uende kuwaambia watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalema kwamba: Yawe anasema hivi: Mimi nimekwisha kukamata mipango juu yenu, na nimekusudia kuleta hasara juu yenu. Basi kila mumoja arudi kutoka katika njia mbaya, abadilishe mwenendo wake na matendo yake.


Kisha, wewe Zedekia, mufalme wa Yuda, pamoja na wakubwa wa serikali yako na watu wa muji huu ambao watakaoponyoka magonjwa hayo makali pamoja na vita na njaa, nitawatoa katika mikono ya Nebukadneza, mufalme wa Babeli na katika mikono ya waadui zenu wanaovizia maisha yao. Nebukadneza atawaua kwa upanga wala hatawahurumia au kuwaachilia au kuwasamehe. –Ni ujumbe wa Yawe.


Nitawatayarisha waangamizaji wakufikie, kila mumoja akishika silaha yake. Watazikata nguzo zako nzuri za mierezi, na kuzitumbukiza katika moto.


basi, nitayaita makabila yote ya kaskazini pamoja na mutumishi wangu Nebukadneza, mufalme wa Babeli. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nitawaleta waishambulie inchi hii na wakaaji wake pamoja na mataifa yote jirani. Nitawaangamiza kabisa, na kuwafanya kuwa kitu cha kuchukiza, cha kuzomewa na kuzarauliwa milele.


Mpaka wakati gani nitaendelea kuona bendera za vita na kusikia mulio wa baragumu?


Mutangaze kati ya mataifa, munyanyue bendera na kutangaza, musifiche jambo lolote. Museme: Babeli umetekwa, mungu Beli amepatishwa haya. Merodaki amefazaishwa; sanamu zake zimefezeheshwa, miungu yake imefazaishwa.


Kelele za vita zinasikilika katika inchi, kuna uharibifu mukubwa.


Mupandishe bendera ya vita kwa kushambulia kuta za Babeli. Muimarishe walinzi, muweke walinzi, mutayarishe mashambulizi. Yawe amepanga na kutimiza mambo aliyosema juu ya wakaaji wa Babeli.


Pandisha bendera ya vita katika dunia, piga baragumu kati ya mataifa; uyatayarishe mataifa kwa kupigana naye; uziite falme kwa kuishambulia; falme za Ararati, Mini na Askenazi. Weka jemadari juu yake; ulete farasi kama makundi ya nzige.


Sikiliza! Kilio kinasikilika kutoka Babeli! Kishindo cha maangamizi makubwa kutoka inchi ya Wakaldea!


Enyi watu wa kabila la Benjamina, muondoke Yerusalema, mukimbie! Mupige baragumu katika muji Tekoa! Muonyeshe kitambulisho cha vita huko Beti-Keremu, maana hasara na maangamizi makubwa vinakuja kutoka upande wa kaskazini.


Yawe anasema hivi: Muangalie, watu wanakuja toka inchi ya kaskazini; taifa kubwa linajitayarisha kutoka mbali kwa mwisho wa dunia.


Kisha nikamusikia Yawe akisema kwa sauti kubwa: Mujongee karibu ninyi mutakaouazibu muji huu. Mukuje na silaha zenu za kuangamiza.


Watu sita wakakuja kutoka upande wa mulango wa juu unaoelekea upande wa kaskazini, kila mumoja na silaha yake ya kuangamiza katika mukono wake. Pamoja nao, kulikuwa mutu mumoja ambaye alikuwa amevaa nguo ya kitani, naye ana chupa la wino. Wakaingia ndani ya hekalu, wakasimama pembeni ya mazabahu ya shaba.


Siku hiyo, kutasikilika kilio kutoka Mulango wa Samaki, maombolezo kutoka Mutaa wa Pili, na mulio mukubwa kutoka katika milima. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Lile gari linalokokotwa na farasi weusi linakwenda upande wa kaskazini, lile linalokokotwa na farasi weupe linakwenda upande wa magaribi, na lile linalokokotwa na farasi wa kijivujivu linakwenda upande wa kusini.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ