Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 4:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Mutoe tangazo, mupashe habari huko Yerusalema! Mupige baragumu kila pahali katika inchi! Mulalamike, mukisema: Mukusanyike pamoja! Mukimbilie katika miji yenye kuzungukwa na kuta!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 4:5
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kila mara itakapopita kwenu itawapata; nayo itapita kila asubui, muchana na usiku. Kusikia ujumbe huu tu kutakuwa kitisho.


Sikiliza maneno ya agano hili, kisha uende kuyatangazia watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalema.


Lakini Nebukadneza, mufalme wa Babeli alipofika, kuishambulia inchi hii, tuliamua kuja Yerusalema kwa kuepuka waaskari wa Wakaldea na wa Wasuria. Kwa hiyo sasa tunaishi katika muji Yerusalema.


Muwatangazie wazao wa Yakobo; muwaambie hao watu wa Yuda hivi:


Enyi watu wa kabila la Benjamina, muondoke Yerusalema, mukimbie! Mupige baragumu katika muji Tekoa! Muonyeshe kitambulisho cha vita huko Beti-Keremu, maana hasara na maangamizi makubwa vinakuja kutoka upande wa kaskazini.


Watu wanauliza: Kwa nini sisi tunakaa tu hapa? Tukusanyike, tuingie katika miji yenye kuzungukwa na kuta, tuangamie kule! Yawe, Mungu wetu, amekusudia tuangamie, ametupa maji yenye sumu tukunywe, kwa sababu tumemukosea yeye.


Yawe akajibu na kusema hivi: Ni kwa sababu wamekataa kushika sheria yangu niliyowapa, wamekataa kutii sauti yangu na kufuata mapenzi yangu.


Baragumu imepigwa na kuwafanya wote wakuwe tayari. Lakini hakuna anayekwenda kwa vita, kwa maana kasirani yangu iko juu ya watu wote.


Mupige baragumu! Adui anakuja kama tai kuishambulia nyumba ya Yawe, kwa sababu wamelivunja agano langu na kuiasi sheria yangu.


Mupige baragumu kule Sayuni; mupige kelele la kujulisha hatari kule juu ya mulima mutakatifu! Mutetemeke enyi wakaaji wa Yuda, maana siku ya Yawe inakuja, siku hiyo iko karibu!


Baragumu ya vita inalia katika muji bila kutia watu hofu? Muji unaweza kupatwa na hasara ambayo haikuletwa na Mungu?


Simba akinguruma, ni nani asiyeogopa? Bwana wetu Yawe akisema, ni nani atakataa kuutangaza ujumbe wake?


Tengeneza baragumu mbili kwa feza iliyofuliwa. Utatumia baragumu hizo wakati wa kuwaita watu na wakati wa kuvunja kambi.


Baragumu zote mbili zikipigwa pamoja, watu wote watakusanyika karibu nawe mbele ya mulango wa hema la mukutano.


Yoshua pamoja na Waisraeli wakawapiga na kuwaangamiza wote, na wachache wao walioponyoka wakakimbilia kwenye miji yao yenye kuta.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ