Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 4:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Enyi watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalema, mujitahiri, mukiondoa govi za mioyo yenu, mupate kujitoa kwa Yawe. Kama si vile, kasirani yangu itawaka kama moto, nayo itaunguza wala hakuna atakayeizimisha, kwa sababu ya matendo yenu maovu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 4:4
36 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa sababu wameniacha mimi na kufukizia miungu mingine ubani kusudi wanikasirikishe sana kwa kazi zote za mikono yao, basi kasirani yangu itamwagika juu ya pahali hapa wala haitatulizwa.


Mungu anayekuwa mwangaza wa Israeli atakuwa kama moto. Mutakatifu wa Israeli atakuwa ulimi wa moto ambao kwa siku moja utateketeza kila kitu, miiba yake na michongoma zake pamoja.


Kweli, pahali pa kumuteketeza mufalme wa Asuria pamekwisha kutayarishwa muda murefu uliopita. Pahali penyewe ni shimo kubwa na pana. Kuna moto na kuni kwa uwingi. Yawe ataupulizia pumzi yake kama kijito cha kiberiti na kuuwasha.


Amuka, ewe Yerusalema! Amuka usimame wima! Yawe amekukunywesha kikombe cha kasirani yake, nawe umekikunywa mpaka tone la mwisho, mpaka ukayumbayumba.


Nitawafanya muwatumikie waadui zenu katika inchi musiyoijua kwa sababu hasira yangu imewaka kama moto usiozimika hata milele.


Enyi jamaa ya Daudi, Yawe anasema hivi: Kila asubui muamue maneno kufuatana na sheria yangu, muwakomboe wote walionyanganywa mali zao toka katika mikono ya watesaji. Kama si vile, hasira yangu itawaka kama moto, wala hakuna atakayeweza kuizimisha, kwa sababu ya matendo yenu maovu.


Mimi mwenyewe nitapigana nawe kwa mukono wangu wenye nguvu na uwezo, kwa hasira, ukali na kasirani kubwa.


Angalia, zoruba kali kutoka kwa Yawe; kasirani yake imeamuka, upepo mukali utapiga kichwa cha mwovu.


Labda maombi yao yatamufikia Yawe na kila mumoja wao ataacha mwenendo wake mubaya kwa maana hasira na kasirani ambavyo Yawe amesema juu ya watu hawa ni kubwa sana.


Yawe hakuweza kuvumilia tena matendo yenu maovu na mambo ya kuchukiza muliyotenda; ndiyo maana inchi yenu imekuwa ukiwa, jangwa, laana na bila wakaaji, kama inavyokuwa mpaka leo.


Wamisri, Wayuda, Waedomu, Waamoni, Wamoabu na wakaaji wote wa jangwa wanaonyoa nywele zote za pembenipembeni ya kichwa. Maana watu hawa wote na Waisraeli wote hawajatahiriwa mioyo yao.


Yawe ameonyesha kabisa kasirani yake, aliimwanga hasira yake kali, aliwasha moto huko katika Sayuni ambao uliteketeza misingi yake.


Nitakuhukumu kama vile wanawake wanaovunja ahadi ya ndoa au wauaji wanavyohukumiwa; nitakuhukumu kwa azabu ya kifo kwa hasira na kwa ajili ya wivu.


Mutupilie mbali zambi mulizonitendea; mujipatie moyo na roho mupya. Enyi Waisraeli, mutakufa kwa sababu gani?


Kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– nitawatawala kwa mukono wenye nguvu, kwa ukali na kuwamwangia kasirani yangu.


Wewe mwanadamu, ulie na kuomboleza upanga huo umenyooshwa juu ya watu wangu, juu ya wakubwa wote wa Waisraeli. Wataangamizwa kwa upanga pamoja na watu wangu. Ujipigepige kifua kwa huzuni.


Ewe Yerusalema, matendo yako machafu yamekuchafua. Ingawa nilijaribu kukutakasa, mwenyewe ulibaki muchafu. Basi, hautatakasika tena mpaka nitakapotuliza hasira yangu juu yako.


Damu hiyo nimeiacha huko juu ya jiwe kusudi isifunikwe, nipate kuamusha kasirani yangu na kulipiza kisasi.


Mumelichafua hekalu langu kwa kuruhusu waingie humo watu wasiotahiriwa, watu wasionitii mimi, wakati mafuta na damu vinatolewa kwa ajili yangu. Hivyo, ninyi watu wangu mumelivunja agano langu kwa machukizo yenu yote.


Anayekuwa mbali sana atakufa kwa ugonjwa mukali. Anayekuwa karibu atauawa kwa upanga. Atakayekuwa amebaki na kuponyoka hayo mawili atakufa kwa njaa. Ndivyo nitakavyotimiza kasirani yangu juu yao.


Kwa sababu ya mambo hayo watasikia uzito wa kasirani yangu. Sitamwacha hata mutu mumoja aponyoke wala sitamwonea huruma mutu yeyote. Hata wakinililia kwa sauti kubwa mimi sitawasikiliza.


basi nami nitapingana nanyi kwa hasira kali, na kuwaazibu mimi mwenyewe mara saba zaidi kwa ajili ya zambi zenu.


wakitambua kwa nini nilipingana nao na kuwapeleka katika inchi ya waadui zao, kama kweli moyo wao mugumu ukinyenyekea na kutubu uovu wao,


Mutafute Yawe, nanyi mutaishi! Kama sivyo, atawatokea wazao wa Yosefu kama moto; moto utawateketeza wakaaji wa Beteli na hakuna mutu atakayeweza kuuzimisha.


mbele hamujapeperushwa mbali kama maganda, mbele haijawafikia siku ya hasira kali ya Yawe, mbele haijawafikia siku ya kasirani ya Yawe.


Kutahiriwa kuna mafaa kama ukitii Sheria. Lakini usipotii Sheria, wewe unahesabiwa kama mutu asiyetahiriwa.


Kwa hiyo, mutahiri magovi ya mioyo yenu, musikuwe wagumu tena.


Yawe, Mungu wenu, atawafanya ninyi na wazao wenu mukuwe na moyo wa utii kusudi mumupende yeye kwa moyo wenu wote na roho yenu, mupate kuishi.


Hasira yangu imewaka moto, inachoma mpaka chini kuzimu, itateketeza dunia na vinavyokuwa ndani yake, itaunguza misingi ya milima.


Katika kuungana naye, mumetahiriwa wala si kwa mikono ya watu, lakini mumetahiriwa na Kristo, na kutahiriwa kule kumewakomboa toka katika hali zaifu ya kimwili.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ