Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 4:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 ukiapa kwa ukweli, kwa kufuatana na sheria, na kwa haki, kwa kusema “Kama vile Yawe anavyoishi”, halafu mataifa yatapata baraka kutoka kwangu, na kutukuzwa kwa sababu yangu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 4:2
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kutokana na wazao wako mataifa yote katika dunia yatabarikiwa kwa sababu wewe umeitii amri yangu.”


Solomono akamwambia: “Ulimwonyesha wema mwingi mutumishi wako Daudi, baba yangu, kwa sababu alikutumikia kwa uaminifu, kwa haki na kwa moyo wa usawa; na umedumisha mema yako kwa kumupa mwana anayeikaa sasa kwenye kiti chake cha kifalme.


Jina la mufalme litukuzwe siku zote; utukufu wake udumu muda wote jua litakapokuwa. Kwake mataifa yote yabarikiwe; watu wote wamwite mwenye heri!


Ee mufalme mukubwa, mupenda haki, umesimamisha usawa katika Israeli; umeleta sheria na haki.


Mimi nimeapa kwa nafsi yangu, ninachosema ni ukweli, neno langu halitarudi nyuma: kila mwanadamu atanipigia magoti, kila mutu atafanya kiapo.


Lakini wazao wa Israeli watapata ushindi toka kwa Yawe na kufurahi.


Basi, mwenye kujitakia baraka katika inchi, atajitakia baraka kwa Mungu wa kweli. Mwenye kuapa katika inchi hii, ataapa kwa Mungu wa kweli. Maana taabu za zamani zimepita zimetoweka kabisa mbele yangu.


Lakini Yawe ni Mungu wa kweli, Mungu Mwenye Uzima, mufalme wa milele. Akikasirika, dunia inatetemeka, mataifa hayawezi kuvumilia hasira yake.


Lakini kisha kuwaongoa, nitawahurumia tena; nitalirudisha kila taifa katika sehemu yake na katika inchi yake.


Na kama watajifunza mwenendo wa watu wangu kwa moyo wote, wakiapa kwa jina langu, wakisema “Kama vile Yawe anavyoishi”, kama vile walivyowafundisha watu wangu kuapa kwa jina la mungu Bali, basi watastawi katikati ya watu wangu.


Ee Yawe! Wewe ndiwe nguvu yangu na upango wangu; wewe ni kimbilio langu wakati wa taabu. Mataifa toka pande zote za dunia yatakufikia na kusema: Miungu ya babu zetu ilikuwa ya uongo, ilikuwa ya bure, isiyofaa kitu.


Wakati huo, Yerusalema utaitwa “Kiti cha Kifalme cha Yawe”, na mataifa yote yatakusanyika humo mbele yangu. Hawatafuata tena ugumu wao unaotokana na matendo yao mabaya.


Nao muji huu utakuwa kwangu jina la furaha, sifa na utukufu mbele ya mataifa yote katika dunia ambayo yatasikia juu ya mema yote ninayowafanyia. Mataifa yataogopa na kutetemeka kwa sababu ya mema na amani nitakazouletea muji huu wa Yerusalema.


Ingawa watu wake wanaapa kwa nafsi ya Yawe, viapo vyao ni vya uongo.


Lakini mugeuze mwenendo wenu na matendo yenu. Mufuate sheria yangu kati yenu.


Siku zinakuja ambapo nitawaazibu wote waliotahiriwa kimwili tu. –Ni ujumbe wa Yawe.– Ni kusema nitawaazibu:


Maana, nitalifanya jina la Bali lisitajike tena katika kinywa chako.


Lakini hata sasa, munirudilie kwa moyo wote, kwa kufunga kula, kwa kulia na kuomboleza. –Ni ujumbe wa Yawe.–


na kuwafanya wakae katika Yerusalema. Wao watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao; nitatawala juu yao kwa uaminifu na haki.


Watu wa mataifa katika dunia yote tokea upande jua linapopanda mpaka upande jua linaposhuka wanalitukuza jina langu. Kila pahali wananifukizia ubani na kunitolea sadaka zinazokubaliwa; maana jina langu linatukuzwa kati yao.


Kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Anayetaka kujivuna, ajivune kwa ajili ya Bwana.”


Lakini, kama Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Anayetaka kujivuna, ajivune kwa ajili ya Bwana.”


Vilevile Maandiko Matakatifu yalisema tangu zamani kwamba watu wa mataifa mengine watahesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya imani yao. Kwa sababu Mungu alipasha kwanza Habari Njema hii kwa Abrahamu: “Kwa njia yako mataifa yote yatabarikiwa.”


Mumwogope Yawe, Mungu wenu, mumutumikie, muambatane naye na kuapa kwa jina lake.


Mambo haya yote yatakapowapata huko, kisha mukipata taabu, mutamurudilia Yawe na kumutii.


Mutamwogopa Yawe, Mungu wenu, mutamutumikia yeye peke yake na kuapa katika jina lake peke yake.


Sisi ndio wenye kutahiriwa kwa kweli, maana tunamwabudu Mungu kwa uongozi wa Roho wake na kujivuna kwa ajili ya Yesu Kristo. Sisi hatuweki tumaini letu katika mambo ya kimwili.


Kwa hiyo, kaa hapa usiku wote, na kesho asubui tutaona kama atakubali kukutunza au hapana. Ikiwa atakutunza ni vizuri. Kama vile Yawe anavyoishi, akikataa, mimi nitakutunza. Lala hapa mpaka asubui.”


Daudi akaapa vilevile: “Hakika baba yako anajua vizuri kwamba nimepata kukubaliwa mbele yako. Anafikiri kukuficha juu ya jambo hili kusudi usihuzunike atakapolitenda. Lakini kweli, kama Yawe anavyoishi na kama wewe mwenyewe unavyoishi, kati yangu na lufu kuna hatua moja tu!”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ