Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 4:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 lakini ni upepo mukali sana unaotoka kwangu. Ni mimi Yawe nitakayetoa hukumu juu yao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 4:12
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Atawanyeshea waovu makaa ya moto na kiberiti; upepo mukali utakuwa ndio azabu yao.


Nami nitawahukumu Waisraeli kwa ajili ya uovu wao wote, kwa maana waliniacha mimi na kuifukizia miungu mingine ubani na kuabudu sanamu walizojitengenezea wenyewe.


Wakati huo, wataambiwa hivi watu hawa pamoja na muji Yerusalema: Upepo wenye kuunguza kutoka vilele vya milima katika jangwa utawavumia watu wangu. Huo si upepo mudogo wa kupepeta ngano,


Angalia! Adui anakuja akivuma kama mawingu. Magari yake ya vita ni kama zoruba, nao farasi wake wa vita wanaruka mbio kuliko tai. Ole kwetu! Tumeangamia!


Yawe anasema hivi: Nitavumisha upepo wa kuangamiza juu ya Babeli na juu ya wakaaji wa Kaldea.


Basi, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitapingana nanyi nami nitatimiza hukumu zangu juu yenu mbele ya mataifa.


Hata kama Efuraimu atastawi kama nyasi, mimi Yawe nitavumisha upepo mukali wa mashariki, upepo utakaotokea kule katika jangwa, nao utakausha visima vyake, chemichemi zake zitakauka. Vitu vyake vyote vya bei kali vitaharibiwa.


Kisha wanasonga mbele kama upepo, wanapita na kufanya makosa. Nguvu zao ndio mungu wao!


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ