Yeremia 4:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20021 Yawe anasema hivi: Ukitaka kurudi, ee Israeli, unirudilie mimi. –Ni ujumbe wa Yawe.– Ukiviondoa vitu vyako vya kuchukiza mbele yangu, usipotangatanga huko na huko, အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
Asa aliposikia maneno haya, ni kusema unabii wa Azaria mwana wa Odedi, yakamutia moyo. Akaondoa sanamu zote za kuchukiza katika inchi yote ya Yuda na ya Benjamina, na kutoka katika miji yote aliyoteka katika inchi ya milima ya Efuraimu. Na kisha akatengeneza upya mazabahu ya Yawe iliyokuwa katika baraza la nyumba ya Yawe.
Niliwapelekea tena na tena watumishi wangu wote, ni kusema manabii wawaambie kila mumoja wenu aachane na mwenendo wake mwovu, abadilishe matendo yake na kuacha kuifuata na kuitumikia miungu mingine. Na kwamba mukifanya hivyo mutakaa katika inchi niliyowapa ninyi na babu zenu. Lakini ninyi hamukunitegea sikio wala hamukunisikiliza.