Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 39:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Katika mwezi wa kenda wa mwaka wa kenda wa utawala wa Zedekia mufalme wa Yuda, Nebukadneza mufalme wa Babeli alifika na waaskari wake wote kuushambulia Yerusalema, akauzunguka kwa vita.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 39:1
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa hiyo, Yawe alimuleta mufalme wa Wakaldea ambaye aliwaangamiza vijana wao kwa upanga hata ndani ya Pahali Patakatifu; wala hakumuhurumia mutu yeyote akuwe kijana au binti, muzee au muzaifu. Wote Yawe aliwatia katika mikono yake.


Yawe akamutolea Yeremia ujumbe katika mwaka wa kumi wa utawala wa Zedekia mufalme wa Yuda, ambao ulikuwa mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Nebukadneza.


Yawe akamutolea Yeremia ujumbe huu wakati Nebukadneza, mufalme wa Babeli, pamoja na waaskari wake wote na falme zote za dunia zilizokuwa chini ya utawala wake, vilevile na watu wote walipokuwa wakiushambulia Yerusalema na miji mingine yote ya kandokando yake:


Nitawaamuru nao wataurudia katika muji huu. Wataushambulia, watauteka na kuuteketeza kwa moto. Nitaifanya miji ya inchi ya Yuda kuwa ukiwa bila wakaaji. –Ni ujumbe wa Yawe.


Maana Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Kama vile hasira yangu na kasirani yangu ilivyowapata wakaaji wa Yerusalema, ndivyo kasirani yangu itakavyowapata ninyi, kama mutakwenda Misri. Mutakuwa kitu cha kutukaniwa, kitisho, laana na haya. Hamutaona tena nafasi hii.


Zedekia alikuwa na umri wa miaka makumi mbili na mumoja alipoanza kutawala. Alitawala kwa muda wa miaka kumi na mumoja akiwa kule Yerusalema. Mama yake aliitwa Hamutali binti wa Yeremia, mukaaji wa muji wa Libuna.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Mukate miti na kulundika udongo, kwa kuweza kupandia ndani ya Yerusalema. Muji huu unapaswa uazibiwe, maana hamuna lolote ndani yake isipokuwa ukorofi tu.


Siku ya tano ya mwezi wa kumi, mwaka wa kumi na mbili tangu tulipopelekwa katika uhamisho, mutu mumoja aliyetoroka kutoka Yerusalema alikuja kwangu, akasema: Muji Yerusalema umetekwa!


Nawe utwae bamba la chuma. Ulisimamishe likuwe kama ukuta wa chuma kati yako na muji. Kisha utaelekezea muji huo uso wako nao utashambuliwa na utaushambulia. Hiki kitakuwa kitambulisho kwa taifa la Waisraeli.


Katika mwaka wa makumi mbili na tano tangu tulipopelekwa katika uhamisho, siku ya kumi ya mwezi wa kwanza, siku hiyo Yawe alinijaza uwezo wake. Ilikuwa mwaka wa kumi na ine tangu pale Yerusalema ulipotekwa.


Kisha kutimia kwa wakati wa kushambuliwa kwa muji wa Yerusalema, utachoma sehemu moja ya tatu ya nywele zako katikati ya muji. Sehemu ingine moja ya tatu utaikatakata kwa upanga ukiuzunguka muji. Sehemu ya tatu ya mwisho utaipeperusha kwa upepo, nami nitauchomoa upanga wangu na kuwafuatilia nyuma.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Siku za mafungo ya kula chakula ya mwezi wa ine, mwezi wa tano, mwezi wa saba na mwezi wa kumi, zitakuwa nyakati za furaha na shangwe; zitakuwa sikukuu za shangwe kwa watu wa Yuda. Basi, mupende ukweli na amani.


“Yawe atawapeleka ninyi na mufalme wenu mutakayejichagulia, mpaka kwa taifa ambalo ninyi hamukulijua wala wazee wenu. Na huko mutatumikia miungu mingine ya miti na mawe.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ