Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Zedekia, nitakugeuzia wewe mwenyewe silaha unazozitumia kwa kupigana na mufalme wa Babeli na waaskari wake wanaozunguka inje ya kuta za muji wenu. Nitazikusanya silaha zile katikati ya muji huu.
Mutu atakayebaki katika muji huu atauawa kwa vita au kwa njaa au kwa magonjwa makali. Lakini mutu atakayetoka inje ya muji huu na kujitoa kwa Wababeli wanaozunguka ukuta wake, ataishi; kweli ataokoa maisha yake.
Yawe anasema hivi juu ya mufalme anayetawala katika kiti cha kifalme cha Daudi, na juu ya watu wote wanaokaa katika muji huu, ndio wandugu zenu ambao hawakuondoka kwenda pamoja nanyi katika uhamisho:
Lakini usipojitoa mwenyewe na kujitia katika mikono ya wakubwa wa mufalme wa Babeli, basi, muji huu utatekwa na Wakaldea nao watauteketeza kwa moto, nawe hautaweza kujiepusha toka katika mikono yao.