mufalme Zedekia alimwita na kumukaribisha kwake. Mufalme akamwuliza kwa siri wakiwa katika nyumba yake: Kuna neno lolote kutoka kwa Yawe? Yeremia akamujibu: Ndiyo, kuko. Kisha akaendelea kusema: Wewe utatiwa katika mikono ya mufalme wa Babeli.
Wake wako wote na watoto wako watapelekwa kwa Wakaldea, nawe mwenyewe hautaponyoka. Utakamatwa mateka na mufalme wa Babeli na muji huu utateketezwa kwa moto.
Kama wakubwa wakisikia kwamba nimeongea nawe, kisha wakikuja na kukuambia: Basi utuambie, ulizungumuza nini na mufalme. Usitufiche chochote nasi hatutakuua;