Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 38:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Yawe anasema hivi: Yeyote atakayebaki katika muji huu atakufa kwa vita, njaa na ugonjwa mukali; lakini yule atakayeondoka na kujitoa kwa Wakaldea, ataishi. Maisha yake yatatekwa naye ataishi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 38:2
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Zedekia, nitakugeuzia wewe mwenyewe silaha unazozitumia kwa kupigana na mufalme wa Babeli na waaskari wake wanaozunguka inje ya kuta za muji wenu. Nitazikusanya silaha zile katikati ya muji huu.


Yawe anasema hivi: Na kama vile wanavyozitendea zile tini mbaya, tini zinazokuwa mbaya hata hazifai kukuliwa, ndivyo nitakavyowatendea mufalme Zedekia wa Yuda, wakubwa wa serikali yake pamoja na watu wengine wote wa Yerusalema waliobaki katika inchi hii, na vilevile wale ambao walihamia katika inchi ya Misri.


Lakini watu wa taifa lolote litakalobeba kwenye shingo nira mufalme wa Babeli atakayolazimisha kubeba na kumutumikia, nitawaacha wakae katika inchi yao, walime udongo na kuishi humo. –Ni ujumbe wa Yawe.


Kwa nini wewe na watu wako munataka kufa kwa vita, njaa na magonjwa makali? Maana, hivi ndivyo Yawe alivyosema juu ya yale yatakayolipata taifa lolote litakalokataa kumutumikia mufalme wa Babeli.


Yawe anasema hivi juu ya mufalme anayetawala katika kiti cha kifalme cha Daudi, na juu ya watu wote wanaokaa katika muji huu, ndio wandugu zenu ambao hawakuondoka kwenda pamoja nanyi katika uhamisho:


Nitawashambulia kwa vita, njaa na magonjwa makali. Nitawafanya kuwa kitu cha kuchukiza kwa falme zote za dunia; nitawafanya kuwa mufano wa kutumia kwa kutoa laana. Mutakuwa kitu cha kushangaza, cha kuzarauliwa na cha kuzomewa kati ya mataifa yote nitakapowasambaza.


Kwa hiyo, Yawe anasema hivi: Ninyi hamukunitii juu ya kuwapatia wandugu zenu Waisraeli uhuru. Basi, nami vilevile nitawapatia ninyi uhuru: uhuru wa kuuawa kwa upanga katika vita, kuuawa kwa ugonjwa mukali na kwa njaa. Nitawafanya ninyi kuwa kitambulisho cha kuogopesha kwa falme zote katika dunia.


Maana, kweli nitakuokoa na hautauawa kwa vita; utapata faida ya kuokoa maisha yako kwa sababu umeniamini mimi. –Ni ujumbe wa Yawe.


Watu wote wenye nia ya kwenda kukaa Misri watakufa kwa njaa na ugonjwa mukali wala hakuna hata mumoja wao atakayebaki au kuponyoka kutokana na hasara nitakayowaletea.


Basi, mujue hakika kwamba mutauawa kwa vita, kwa njaa na kwa ugonjwa mukali katika inchi ile munayotaka kwenda kukaa ndani yake.


Nitawaazibu wale wanaokaa katika inchi ya Misri kama nilivyouazibu Yerusalema, kwa vita, njaa, na ugonjwa mukali.


Wewe unajitakia wewe mwenyewe mambo makubwamakubwa? Usiyatafute! Achana nayo, maana ninaleta maangamizi juu ya wanadamu wote. Pato lako ni hili: nitayaokoa maisha yako kila nafasi utakapokwenda. –Ni ujumbe wa Yawe.


Lakini Bwana wetu Yawe anasema: Tena nitauazibu Yerusalema kwa mapigo yangu mane ya hukumu kali: vita, njaa, nyama wakali na ugonjwa mukali, nipate kuangamiza watu na nyama ndani yake!


Bwana wetu Yawe akaniambia hivi: Upige mikono, piga kishindo kwa muguu na kusema: Ole kwenu Waisraeli kwa sababu ya machukizo yenu yote; kwa sababu mutakufa kwa upanga, njaa na kwa ugonjwa mukali.


Inje kuna kifo kwa upanga na ndani ya muji kuna ugonjwa mukali na njaa. Wanaokuwa katika vijiji watakufa kwa upanga; wanaokuwa katika muji wataangamizwa na njaa na ugonjwa mukali.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ