Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 38:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Lakini usipojitoa mwenyewe na kujitia katika mikono ya wakubwa wa mufalme wa Babeli, basi, muji huu utatekwa na Wakaldea nao watauteketeza kwa moto, nawe hautaweza kujiepusha toka katika mikono yao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 38:18
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

na Yoyakini mufalme wa Yuda alijitoa kwa mufalme wa Babeli, yeye mwenyewe pamoja na mama yake, watumishi wake, wakubwa na majemadari wake. Mufalme wa Babeli aliwapeleka kama wafungwa katika mwaka wa nane wa kutawala kwake.


Nimeamua kuleta hasara juu ya muji huu wala siyo mema. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nitautoa katika mikono ya mufalme wa Babeli, naye atauteketeza kwa moto.


Lakini kama taifa lolote au utawala wowote hautajiweka chini ya mamlaka ya Nebukadneza mufalme wa Babeli, na kukataa kubeba katika shingo yao zile nira atakazowalazimisha kubeba, basi nitaliazibu taifa hilo kwa vita, njaa na magonjwa makali mpaka nitakapoliangamiza kabisa kwa njia yake. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Na Wakaldea watarudi kuushambulia muji huu. Watauteka muji na kuuteketeza kwa moto.


Wake wako wote na watoto wako watapelekwa kwa Wakaldea, nawe mwenyewe hautaponyoka. Utakamatwa mateka na mufalme wa Babeli na muji huu utateketezwa kwa moto.


Yawe anasema hivi: Hakika muji huu utatiwa katika mikono ya waaskari wa mufalme wa Babeli na kutekwa.


(Basi wakubwa hawa wote wa mufalme wa Babeli waliingia na kukaa kwenye mulango wa katikati: Nergali-Sarezeri, Samgari-Nebo, Sarsekimu jemadari mukubwa wa na Nergali-Sarezeri mukubwa wenye maarifa, pamoja na wakubwa wengine wote wa mufalme wa Babeli.)


Wakaldea waliichoma kwa moto nyumba ya kifalme na nyumba za watu; vilevile walizibomoa kuta za Yerusalema.


Lakini nitatandaza wavu wangu juu yake, naye atanaswa katika mutego wangu. Nitamupeleka Babeli, inchi ya Wakaldea; naye akiwa huko atakufa bila kuiona inchi hiyo.


Lakini yule mufalme mupya alimwasi mufalme wa Babeli kwa kuwatuma wajumbe Misri kuomba farasi na waaskari wengi. Mufalme huyo atashinda? Anayefanya hivyo na kuvunja agano lake ataweza kuepuka azabu?


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ