Mufalme alipomwona malkia Esteri akisimama katika kiwanja, Esteri akapata kukubaliwa mbele yake, naye akamunyooshea fimbo ya zahabu aliyokuwa akishika katika mukono wake. Esteri akakaribia, akagusa incha ya fimbo.
Mufalme Ahasuero akawaambia malkia Esteri na Mordekayi, yule Muyuda: “Muangalie! Nimemupa Esteri mali ya Hamani, naye wamekwisha kumutundika kwa sababu ya shauri lake baya juu ya Wayuda.
Basi, Ebedimeleki akatwaa watu hao na kwenda pamoja nao katika nyumba ya kifalme, wakaingia katika gala ya nyumba ya kifalme; Ebedimeleki akatwaa nguo zilizopasukapasuka na kuchakaa, akaziteremushia Yeremia ndani ya kisima kwa kamba.
Lakini Ebedimeleki, towashi Mwetiopia aliyetumika katika nyumba ya kifalme, alipata habari kwamba walikuwa wamemutia Yeremia katika kisima. Wakati huo mufalme alikuwa anafanya baraza kwenye mulango wa Benjamina.
Bwana wangu mufalme, watu hawa wamefanya kitu kibaya. Wamemutia yule nabii Yeremia katika kisima ambamo kwa kweli atakufa kwa njaa, kwa maana hakuna chakula tena katika muji.