na Yoyakini mufalme wa Yuda alijitoa kwa mufalme wa Babeli, yeye mwenyewe pamoja na mama yake, watumishi wake, wakubwa na majemadari wake. Mufalme wa Babeli aliwapeleka kama wafungwa katika mwaka wa nane wa kutawala kwake.
Neno hili lilimufikia Yeremia kutoka kwa Yawe, wakati mufalme Zedekia alipowatuma Pashuri mwana wa Malkia, na kuhani Zefania mwana wa Masea kwa kumwambia Yeremia hivi:
Yawe anasema hivi: Kama vile ninavyoishi, hata kama wewe Konia mwana wa Yoyakimu, mufalme wa Yuda, ungekuwa wa lazima kwangu kama vile pete yangu ya muhuri ninayovaa kwa mukono wangu wa kuume, ningekuvua.
Mbona huyu mutu Konia, amekuwa kama chungu kilichovunjika, ambacho kinazarauliwa na kutupwa inje? Kwa nini yeye na watoto wake wamefukuzwa, wametupwa katika inchi wasiyoijua?
Ilikuwa nyuma ya Nebukadneza mufalme wa Babeli kuwahamisha Yekonia mufalme wa Yuda mwana wa Yoyakimu, pamoja na wakubwa wa inchi ya Yuda na wafundi bora na wafuaji wa vyuma kutoka Yerusalema na kuwapeleka Babeli. Yawe akanionyesha vikapu viwili vya matunda ya tini vimewekwa mbele ya hekalu la Yawe.
Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Kwenda usemezane na Zedekia, mufalme wa Yuda. Umwambie kwamba mimi Yawe ninasema hivi: Nimeutia muji huu katika mikono ya mufalme wa Babeli, naye atauteketeza kwa moto.
Katika mwaka wa makumi tatu na saba tangu Yoyakinu mufalme wa Yuda alipopelekwa katika uhamisho, siku ya makumi mbili na tano ya mwezi wa kumi na mbili, Ewili-Merodaki akakuwa mufalme wa Babeli. Mwaka uleule alipofanywa mufalme, alimusamehe Yoyakinu mufalme wa Yuda, akamwondoa katika kifungo.