Lakini yule mufalme mupya alimwasi mufalme wa Babeli kwa kuwatuma wajumbe Misri kuomba farasi na waaskari wengi. Mufalme huyo atashinda? Anayefanya hivyo na kuvunja agano lake ataweza kuepuka azabu?
Watu watajaribu kupigana na Wakaldea lakini hiyo itakuwa bure, maana mifereji itajaa maiti za watu ambao nitawaua kwa hasira na kasirani yangu. Kwa vile wamefanya uovu huo wote, mimi nitauacha muji huu.
Vyombo hivyo vitapelekwa Babeli, navyo vitabaki huko mpaka siku nitakapovishugulikia. Hapo ndipo nitakapovirudisha na kuviweka tena pahali hapa. –Ni ujumbe wa Yawe.
Lakini nitatandaza wavu wangu juu yake, naye atanaswa katika mutego wangu. Nitamupeleka Babeli, inchi ya Wakaldea; naye akiwa huko atakufa bila kuiona inchi hiyo.
Hata kama mukiwashinda waaskari wote wa Wakaldea wanaopigana nanyi na kunabaki tu katika mahema yao wale walioumizwa, hao watasimama na kuuteketeza muji huu kwa moto.
Halafu Roho wa Mungu akamujaza Zakaria mwana wa kuhani Yoyada, naye akasimama mbele ya watu kwa pahali palipokuwa juu kidogo, akawaambia: “Yawe anauliza: Kwa nini mumevunja sheria zake? Sasa hamuwezi kufanikiwa! Kwa vile mumemwacha, naye vilevile amewaacha!”
Na muangalie, Mungu mwenyewe ndiye kiongozi wetu na makuhani wake wako na baragumu zao tayari kuzipiga kwa kupana kitambulisho cha kuanza vita juu yenu. Enyi watu wa Israeli, muache kupigana vita na Yawe, Mungu wa babu zenu. Hamuwezi kushinda!”
Lakini kundi la waaskari la Wakaldea liliwafuatilia na kumukamata Zedekia karibu na Yeriko. Kisha kumukamata walimufikisha kwa Nebukadneza, mufalme wa Babeli huko Ribla, katika inchi ya Hamati, naye akamuhukumu.
Aliyahesabu makosa yangu yote akayakusanya pahali pamoja; aliyafunga katika shingo langu kama nira, nikafyonzwa nguvu zangu kwa uzito wake. Yawe aliniweka katika mikono ya watu ambao siwezi kuwapinga.
Naye mutawala wao atabeba muzigo wake juu ya mabega wakati wa usiku, atatoka kupitia ukuta atakaotoboa apate kutoka; atafunika uso wake kusudi asiione inchi kwa macho yake.
Naye Zedekia, mufalme wa Yuda na waaskari wake wote walipowaona, walitoroka. Walitoka inje ya muji usiku, wakipitia katika bustani ya mufalme, kwenye mulango katikati ya kuta mbili, wakatelemukia kwenye bonde la muto Yordani.