Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 32:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Zedekia, mufalme wa Yuda, hataepuka kutiwa katika mikono ya Wakaldea; hakika atatekwa na mufalme wa Babeli, ataonana naye uso kwa uso na kuongea naye kinywa kwa kinywa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 32:4
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha, wewe Zedekia, mufalme wa Yuda, pamoja na wakubwa wa serikali yako na watu wa muji huu ambao watakaoponyoka magonjwa hayo makali pamoja na vita na njaa, nitawatoa katika mikono ya Nebukadneza, mufalme wa Babeli na katika mikono ya waadui zenu wanaovizia maisha yao. Nebukadneza atawaua kwa upanga wala hatawahurumia au kuwaachilia au kuwasamehe. –Ni ujumbe wa Yawe.


Wachungaji hawana makimbilio, wakubwa wa kundi hawataweza kutoroka.


Naye Zedekia, mufalme wa Yuda, pamoja na wakubwa wake, nitawatia katika mikono ya waadui zao, na katika mikono ya watu wanaotaka kuwaua; ni kusema katika mikono ya waaskari wa mufalme wa Babeli ambao wameondoka na kuacha kuwashambulia.


Nawe hautatoroka toka mikono yake, lakini kwa hakika utatekwa na kupelekwa kwake; utaonana na mufalme wa Babeli macho kwa macho, na kusema naye kinywa kwa kinywa; kisha, utakwenda Babeli.


mufalme Zedekia alimwita na kumukaribisha kwake. Mufalme akamwuliza kwa siri wakiwa katika nyumba yake: Kuna neno lolote kutoka kwa Yawe? Yeremia akamujibu: Ndiyo, kuko. Kisha akaendelea kusema: Wewe utatiwa katika mikono ya mufalme wa Babeli.


Lakini usipojitoa mwenyewe na kujitia katika mikono ya wakubwa wa mufalme wa Babeli, basi, muji huu utatekwa na Wakaldea nao watauteketeza kwa moto, nawe hautaweza kujiepusha toka katika mikono yao.


Wake wako wote na watoto wako watapelekwa kwa Wakaldea, nawe mwenyewe hautaponyoka. Utakamatwa mateka na mufalme wa Babeli na muji huu utateketezwa kwa moto.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ