Munachagua mawe laini katika mabonde, na kuyafanya kuwa mungu wenu. Munayamwangia sadaka ya kinywaji na kuyapelekea sadaka ya unga! Mimi nitatulizwa kwa vitu hivyo?
Nitalipiza kisasi mara mbili zaidi juu ya zambi zao na makosa yao, kwa sababu wameichafua inchi yangu na mizoga ya miungu yao yenye kuchukiza, wameijaza inchi yangu na hayo machukizo yao. –Ni ujumbe wa Yawe.
Wao wanauambia muti: “Wewe ni baba yetu”, nalo jiwe: “Wewe ndiwe uliyetuzaa”; kwa maana unanigeuzia mugongo, wala hawakunielekezea uso. Lakini wakati wa shida wanasema: Simama utuokoe!
Niliwaleta katika inchi yenye mboleo, muyafurahie mazao yake na mema yake mengine. Lakini mulipofika tu, muliichafua inchi yangu; inchi niliyowapa ikuwe yenu, mukaifanya chukizo.
Inua macho, uangalie vilele vya vilima! Kuna nafasi ambapo hawajalala nawe? Uliwangoja wapenzi wako kando ya njia, kama mubedui anavyovizia watu katika jangwa. Umeichafua inchi kwa ukahaba wako mubaya sana.
Hao walimuvua nguo zake na kumwacha uchi. Waliwakamata watoto wake, naye mwenyewe wakamwua kwa upanga. Azabu hiyo aliyopata ikakuwa fundisho kwa wanawake wengine.
Watu wangu wanaomba shauri kutoka kwa muti; kijiti chao cha kuaguza ndicho kinachowapa shauri. Nia ya kufanya uzinzi imewapotosha; wamefanya uzinzi kwa kufuata miungu mingine, wakaniacha mimi Mungu wao.
Ole wake mutu anayeambia kipande cha muti: Amuka! au jiwe bubu: Simama! Sanamu inaweza kumufundisha mutu? Angalia imepakwa zahabu na feza, lakini haina uzima wowote.
Lakini mimi ninawaambia: mutu yeyote anayeachana na muke wake, isipokuwa tu kwa sababu ya uzinzi, anamufanya muke yule kuwa muzinzi kama akiolewa tena. Na mutu anayemwoa yule muke aliyefukuzwa, anazini vilevile.