Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 3:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Zaidi ya hayo, Yuda alishuhudia kwamba niliachana na Israeli kwa sababu ya ukahaba wake na kwa kukosa uaminifu kwangu. Lakini hata hivyo, Yuda, dada yake mudanganyifu, hakuogopa; naye vilevile alikwenda na kufanya ukahaba!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 3:8
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Tena alitengeneza pahali pa kuabudia miungu mingine katika milima ya Yuda na kusababisha wakaaji wa Yerusalema kukosa uaminifu na watu wa Yuda kupotoka.


Yawe anasema hivi: Kama nimeachana na mama yako Yerusalema, barua ya kuachana iko wapi? Nilikuwa na deni ya nani kwa kuwauzisha? Mukumbuke kwamba muliuzishwa kwa ajili ya maovu yenu, mama yenu alifukuzwa kwa ajili ya makosa yenu.


Uovu wako utakuazibu; na uasi wako utakuhukumu. Ujue na kutambua kwamba ni vibaya sana kuacha Bwana wako Yawe, Mungu wako, na kutokuwa na woga wangu ndani yako. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi.–


Mume akiachana na muke wake, naye muke akijiendea, na kuolewa na mwingine, mume yule anaweza kumurudilia muke huyo? Kufanya hivyo hakutaichafua inchi kabisa? Wewe Israeli, umefanya ukahaba na wapenzi wengi, sasa unataka kunirudilia mimi? –Ni ujumbe wa Yawe.–


Haujasikia namna watu hawa wanavyosema, kwamba mimi Yawe nimewatupilia mbali watu wa Israeli na watu wa Yuda, jamaa mbili nilizochagua? Wamewazarau watu wangu, hata kuwaona kwamba wao si taifa.


Yawe anauliza: Namna gani nitaweza kukusamehe, ee Yerusalema? Watu wako wameniasi; wameapa kwa majina ya miungu ya uongo. Nilipowashibisha kwa chakula, wao walifanya uzinzi, wakakusanyika kwa uwingi katika nyumba za makahaba.


Dada yako mukubwa ni Samaria, aliyekaa upande wako wa kaskazini pamoja na wabinti zake. Dada yako mudogo ni Sodoma, aliyekaa upande wako wa kusini pamoja na wabinti zake.


Lakini wewe haukutosheka kufuata mienendo yao au kutenda sawa na machukizo yao. Kwa muda mufupi tu ulipotoka kuliko vile wao walivyopotoka katika mienendo yako yote.


Naye Samaria kwa kweli hakutenda hata nusu ya zambi zako. Wewe umefanya machukizo mengi kuliko wao. Ukilinganisha maovu yako na ya dada zako, maovu yao si kitu!


Kila mumoja alimwendea kama wanaume wanavyomwendea kahaba. Ndivyo walivyowaendea Ohola na Oholiba wale wanawake waasherati.


Kwa hiyo nikamutoa katika mikono ya Waasuria wapenzi wake, ambao aliwatamani sana.


Hivi ndivyo Waisraeli watakavyokuwa: watakaa kwa muda murefu bila mufalme au mukubwa; bila sadaka, wala nguzo za sanamu wala vyombo walivyotumia kwa kujua mapenzi ya Mungu.


“Ikiwa mwanaume ameoa muke na kisha hapendezwi naye kwa sababu ameona kwake kitu kisichofaa, basi, huyo mwanaume akimwandikia barua ya kuachana, akimupa na kumufukuza kutoka katika nyumba yake, kisha huyo mwanamuke akiondoka,


kama huyo mume wa pili akimutwaa, akimwandikia barua ya kuachana, akimupa na kumufukuza toka katika nyumba yake, au kama huyo mume wake akikufa,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ