Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 3:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Katika siku ya utawala wa mufalme Yosia, Yawe aliniambia hivi: Umeona jinsi yule Israeli asiyekuwa mwaminifu alivyofanya? Aliniacha, akapanda juu ya kila kilima kirefu na kwenda chini ya kila muti wenye majani mabichi, akafanya ukahaba wake kule!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 3:6
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Walijitengenezea vilevile pahali pa ibada, minara ya kutambikia, na sanamu za Ashera, juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila muti wenye majani mengi.


Yosia alikuwa na umri wa miaka minane alipoanza kutawala, alitawala miaka makumi tatu na mumoja akiwa kule Yerusalema.


Hivyo wakajichafua kwa matendo yao, wakakosa uaminifu kwa Mungu kama wazini.


Lakini Yawe anasema: Mukuje hapa ninyi wana wa wake wachawi; ninyi wazao wa wachawi, wazinzi na makahaba.


Mumeweka vitanda vyenu juu ya milima mirefu, na kwenda kule kwa kutambikia.


Neno la Yawe lilimufikia Yeremia katika mwaka wa kumi na tatu wa utawala wa Yosia mwana wa Amoni, mufalme wa Yuda.


Wameurudilia uovu wa babu zao ambao walikataa kusikiliza maneno yangu; wanaiabudu miungu mingine na kuitumikia. Watu wa Israeli na watu wa Yuda wamevunja agano nililofanya na babu zao.


Watoto wao wanakumbuka mazabahu zao na sanamu za mungu muke, Ashera, zilizowekwa kando ya miti mibichi, juu ya vilele vya vilima


Zaidi ya hayo, Yuda alishuhudia kwamba niliachana na Israeli kwa sababu ya ukahaba wake na kwa kukosa uaminifu kwangu. Lakini hata hivyo, Yuda, dada yake mudanganyifu, hakuogopa; naye vilevile alikwenda na kufanya ukahaba!


Utasitasita mpaka wakati gani, ewe binti usiyekuwa mwaminifu? Maana, mimi nimefanya kitu kipya katika dunia; mwanamuke anamulinda mwanaume.


Kweli, watu wa Israeli na watu wa Yuda, wamekosa kabisa uaminifu kwangu. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Lakini wao hawakunitii wala kunitegea sikio. Lakini wakafuata mashauri yao wenyewe na ugumu wa mioyo yao, wakarudi nyuma pahali pa kusonga mbele.


Umejijengea nafasi yako yenye kuinuka kwa mwanzo wa kila barabara na kujijengea pahali pa kutambikia katika kila kiwanja. Tena wewe haukukuwa kama kahaba maana ulikataa kulipwa.


Sasa basi, ewe kahaba, usikilize neno la Yawe.


Maana nilipowapeleka katika ile inchi niliyoapa kuwapa, kila mara walipoona kilima kirefu au miti ya majani mengi, walianza kutoa matambiko na sadaka zao na kunichokoza. Kulekule walitoa sadaka za harufu nzuri na kutoa sadaka za kinywaji.


Dada yake Oholiba aliona jambo hilo, lakini akazidi kupotoka kuliko yeye katika tamaa yake, na uzinzi wake ulikuwa mubaya kuliko wa dada yake.


Yule mukubwa aliitwa Ohola, na yule mudogo Oholiba. Basi, wote wakakuwa wangu, wakanizalia watoto, wana na wabinti. Basi, Ohola ni Samaria na Oholiba ni Yerusalema!


Watu wangu wamekusudia kuniacha mimi, wakiitwa kusimama wapande juu, hakuna hata mumoja anayeweza.


Wanatambikia kwenye vilele vya milima; wanatoa sadaka kwenye vilima, chini ya miti ya mwalo, migude na mikwaju, maana kivuli chao ni kizuri. Kwa hiyo wabinti wenu wanafanya uzinzi, na bibi-arusi wenu anafanya uasherati.


Hata hivyo, Waisraeli hawakuwasikiliza waamuzi wao, maana walifanya kama wazinzi kwa kufuata miungu mingine na kuinama mbele yao. Wakaacha upesi njia ya babu zao. Babu zao walitii amri za Yawe lakini wao hawakuzitii.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ