Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 3:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Inua macho, uangalie vilele vya vilima! Kuna nafasi ambapo hawajalala nawe? Uliwangoja wapenzi wako kando ya njia, kama mubedui anavyovizia watu katika jangwa. Umeichafua inchi kwa ukahaba wako mubaya sana.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 3:2
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

akavua nguo zake za ujane na kujifunika kitambaa. Kisha akaikaa kwenye mulango wa kuingilia Enaimu, kijiji kilichokuwa katika njia kwenda Timuna. Alifanya hivyo kwa vile aliona kwamba Sela alikwisha kuwa mutu muzima, lakini yeye Tamari hakuoeshwa akuwe muke wake.


Solomono akakuwa na wanawake mia saba, wote wabinti wa kifalme, na wahabara mia tatu. Hao wanawake wakamupotosha.


Vilevile aliharibu pahali pa kuabudia palipokuwa upande wa mashariki ya Yerusalema na kuelekea upande wa mulima wa uharibifu, pahali mufalme wa Israeli alipopajenga kwa ajili ya Astaroti chukizo la Wasidoni, Kemosi chukizo la Moabu na vilevile kwa ajili ya Milkomu chukizo la Waamoni.


Walimwanga damu ya wasiokuwa na kosa, damu ya watoto wao wanaume na wabinti ambao waliwatoa sadaka kwa sanamu za Wakanana, nayo inchi ikachafuliwa kwa uuaji huo.


Yeye anavizia kama munyanganyi, anasababisha wanaume wengi kukosa uaminifu.


Alikuwa mwanamuke wa makelele na mwenye kiburi; miguu yake haitulii ndani ya nyumba:


Waangamizaji wamefika, tokea juu ya milima yote katika jangwa. Upanga wangu unapita kuiangamiza inchi, toka upande mumoja mpaka mwingine, wala hakuna mutu atakayeishi kwa amani.


Yawe anasema: Tangu zamani wewe ulivunja nira yako, ulikata minyororo yako, ukasema: “Sitakutumikia”. Juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila muti wa majani mabichi, ukalala machali kama kahaba.


Namna gani basi unaweza kusema: Mimi sikujichafua wala sikufuata miungu Bali. Ukumbuke vile ulivyotenda zambi kule katika bonde; utambue yale uliyofanya huko! Wewe ni kama mwana wa ngamia, anayetangatanga huko na huko;


Niliwaleta katika inchi yenye mboleo, muyafurahie mazao yake na mema yake mengine. Lakini mulipofika tu, muliichafua inchi yangu; inchi niliyowapa ikuwe yenu, mukaifanya chukizo.


Mume akiachana na muke wake, naye muke akijiendea, na kuolewa na mwingine, mume yule anaweza kumurudilia muke huyo? Kufanya hivyo hakutaichafua inchi kabisa? Wewe Israeli, umefanya ukahaba na wapenzi wengi, sasa unataka kunirudilia mimi? –Ni ujumbe wa Yawe.–


Wewe, kubali tu kosa lako: kwamba umeniasi mimi Yawe, Mungu wako; kwamba chini ya kila muti wenye majani, umeonyesha mapenzi yako kwa miungu mingine, wala haukuitii sauti yangu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Kelele linasikilika juu ya vilima: Waisraeli wanalia na kuomboleza, kwa sababu wamepotoka katika njia zao, wamenisahau mimi Yawe, Mungu wao.


Aliona kwamba ukahaba ni jambo dogo sana kwake. Aliichafua inchi kwa kufanya ukahaba, akiabudu mawe na miti.


Munyoe nywele zenu na kuzitupa, enyi wakaaji wa Yerusalema: mufanye maombolezo juu ya vichwa vya milima, maana, mimi Yawe nimewakataa ninyi, nimewatupilia ninyi kizazi kilichosababisha hasira yangu!


Ulitwaa sehemu ya nguo zako, ukaitumia kwa kupamba pahali pako pa kutambikia na hapo ndipo ukafanyia uzinzi wako. Jambo la namna hiyo halijapata kutokea wala halitatokea hata kidogo!


Maana nilipowapeleka katika ile inchi niliyoapa kuwapa, kila mara walipoona kilima kirefu au miti ya majani mengi, walianza kutoa matambiko na sadaka zao na kunichokoza. Kulekule walitoa sadaka za harufu nzuri na kutoa sadaka za kinywaji.


Kama sivyo, nitamuvua nguo abaki uchi, nitamufanya akuwe sawa vile alivyozaliwa. Nitamufanya akuwe utupu sawa jangwa, akauke sawa inchi kavu. Nitamwua kwa kiu.


Alipokuwa katika jehenamu akiteswa sana, akainua macho, akamwona Abrahamu kwa mbali na Lazaro akiwa pembeni yake.


Muharibu kabisa pahali pote ambapo watu wanaabudia miungu yao kwenye milima mirefu, vilima na chini ya miti yenye majani mabichi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ