Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 27:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Basi, ninyi musiwasikilize manabii wenu, wapiga ramuli wenu, wafasiriaji wenu wa ndoto, waaguzi wenu au wachawi wenu, wanaowaambia kwamba musimutii mufalme wa Babeli.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 27:9
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini, mufalme wa Misri akawaita wenye hekima wake na wachawi. Wale wachawi wa Misri wakafanya vile vile kwa uchawi wao.


Mwana wangu, ukiacha kusikiliza mafundisho, mara moja utapotea mbali na maneno ya maarifa.


Watu wamoja watawaambia ninyi: Muombe shauri kwa mizimu na waaguzi wanaolia kama ndege; kwa sababu ni kawaida watu kuomba shauri kwa miungu yao, na kuomba shauri kwa wafu kwa ajili ya wanaokuwa wazima.


Naye Yawe akaniambia: Hao manabii wanatoa unabii wa uongo kwa jina langu. Mimi sikuwatuma, wala sikuwaamuru, wala sikusema nao. Wanawatabiria maono ya uongo, maaguzi yao hayana maana yoyote, wao wanajitungia uongo wenyewe.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Musisikilize maneno manabii wanaowatabiria; wanawapa matumaini ya uongo. Yale wanayowaambia ni maono ya mioyo yao wenyewe. Hayakutoka katika kinywa cha Yawe.


Mimi nimeyasikia maneno waliyosema hao manabii wanaotabiri uongo kwa jina langu, wakisema: Nimeota ndoto, nimeota ndoto!


Vilevile mimi Yawe ninasema kwamba nitawashambulia manabii wanaotabiri ndoto zao za uongo kwa watu wangu, na kuwapotosha kwa uongo wao na upuuzi wao. Mimi sikuwatuma wala kuwaamuru waende, kwa hiyo hawatawafalia watu hao kitu. –Ni ujumbe wa Yawe!


Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Musikubali kudanganywa na manabii wenu na waaguzi wanaokuwa katikati yenu, wala musisikilize ndoto wanazoota.


Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Wote wataweza kuziona zambi zenu. Kila mutu atajua jinsi munavyokuwa na makosa. Kila kitendo munachotenda kinaonyesha zambi zenu. Ninyi mutapata azabu nami nitawatia katika mikono ya waadui zenu.


Nilipokuwa ninalala, niliona maono haya: Niliona muti murefu sana katikati ya dunia.


Waonaji watafezeheka, waaguzi watapata haya; wote watafunga midomo yao, maana hawatapata jibu lolote kutoka kwa Mungu.


Sanamu zao za kupigia ramuli ni uongo mutupu, na waaguzi wao wanaagua uongo; watabiri wao wanatabiri ndoto danganyifu, na kuwapa watu faraja za bure. Ndiyo maana watu wa Yuda wanatangatanga kama kondoo; wanataabika maana wamekosa muchungaji.


Yawe wa majeshi anasema: Kisha nitawakaribia kwa kuwahukumu. Sitasita kutoa ushuhuda juu ya wachawi, wazinzi, watoa ushuhuda wa uongo, wanaopunja mushahara wa watumishi, wanaowatesa wajane na wayatima, wanaozuia mugeni asipate haki yake na wale wasioniogopa mimi.


Hakika walimusikiliza vizuri kwa sababu aliwashangaza kwa muda wa siku nyingi kwa njia ya uchawi wake.


Mutu asiwadanganye na maneno yasiyokuwa na maana; kwa sababu ya makosa kama hayo, Mungu anawaazibu kwa kasirani yake wale wasiomutii.


“Kukitokea nabii au mutabiri wa kutumia ndoto kati yenu na kuwapatia kitambulisho au ajabu fulani,


Kwa maana mataifa haya ambayo mutairizi inchi yao wanafuata maongozi ya waaguzi na wapiga ramuli; lakini Yawe, Mungu wenu hawaruhusu ninyi kufanya hivyo.


Balamu mwaguzi mwana wa Beori ambaye Waisraeli walimwua alikuwa mumoja wao.


Mwangaza wa taa hautaonekana tena ndani yako. Na hakutasikilika tena kelele la wenye kuoa au kuolewa. Itakutokea vile kwa sababu wachuuzi wako walikuwa wenye uwezo mukubwa katika dunia, nawe umewadanganya watu wote kwa njia ya vitendo vyako vya uchawi.”


Lakini watu wenye woga, wasioamini, wenye machukizo, wauaji, wazinzi, wachawi, wanaoabudu sanamu na wote wanaosema uongo, fungu lao ni katika lile ziwa la moto na ndani ya mawe ya kiberiti yanayowaka moto. Hiki ndicho kifo cha pili.”


Lakini mbali ya muji ule kuna watu wenye kuchukiza, wachawi, wazinzi, wauaji, wanaobudu sanamu na wasema uongo na wote wanaoupenda.


Watu wale hawakuacha hata matendo yao ya uuaji, ya uchawi, ya uasherati na ya wizi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ