Zedekia alikuwa na umri wa miaka makumi mbili na mumoja alipoanza kutawala, alitawala kwa muda wa miaka kumi na mumoja akiwa kule Yerusalema. Mama yake aliitwa Hamutali binti wa Yeremia, mukaaji wa muji wa Libuna.
Yeremia akamwambia Zedekia mufalme wa Yuda, mambo hayohayo, akisema: Mukubali kubeba nira mufalme wa Babeli atakayowalazimisha kubeba. Mumutumikie yeye na watu wake, kusudi mupate kuishi.
Kisha, upeleke ujumbe kwa mufalme wa Edomu, mufalme wa Moabu, mufalme wa Amoni, mufalme wa Tiro na mufalme wa Sidona. Uutume kwa mukono wa wajumbe waliokuja Yerusalema kwa kumwona Zedekia mufalme wa Yuda.
Katika mwaka uleule, maana yake mwaka wa ine wa utawala wa mufalme Zedekia juu ya Yuda, katika mwezi wa tano, Hanania, mwana wa Azuri, nabii kutoka muji Gibeoni, alisema nami katika nyumba ya Yawe. Alisema nami mbele ya makuhani na watu wote, akiniambia kwamba
Yawe akamutolea Yeremia ujumbe katika mwaka wa kumi wa utawala wa Zedekia mufalme wa Yuda, ambao ulikuwa mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Nebukadneza.