Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 26:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Kwa nini umetabiri kwa jina la Yawe, ukisema kwamba nyumba hii itaharibiwa kama ile ya Shilo na muji huu utakuwa ukiwa, bila wakaaji? Na watu wote wakamuzunguka Yeremia katika nyumba ya Yawe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 26:9
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Na alipokuwa angali akisema naye, Amazia akamwambia: “Nyamaza! Tulikufanya wewe kuwa mushauri wa mufalme? Kwa nini uawe?” Nabii akanyamaza, lakini akasema: “Ninafahamu kwamba Mungu ameamua kukuangamiza kwa maana umetenda haya yote, kisha unazarau shauri langu.”


Watatoweka wale wanaopotosha maneno ya mutu katika tribinali, watu wanaowatega waamuzi na wanaosema uongo kwa kuwanyima haki yao wasiokuwa na kosa.


Maana Zedekia, mufalme wa Yuda, alikuwa amemufunga Yeremia akisema: Kwa nini unatabiri na kusema: Yawe anasema hivi: Mimi ninautia muji huu katika mikono ya mufalme wa Babeli, naye atauteka.


Yawe anasema hivi: Katika muji huu ambao munasema kwamba umekuwa ukiwa bila watu wala nyama, katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalema ambazo ni tupu, bila watu wala nyama, humo kutasikilika tena sauti za vicheko, sauti za furaha,


Nawe utamwambia huyo Yoyakimu mufalme wa Yuda kwamba: Yawe anasema hivi: Umekichoma kwa moto kitabu hicho na kuuliza kwa nini Yeremia ameandika kwamba mufalme wa Babeli atakuja kuiharibu inchi hii na kuwaangamiza watu na nyama!


Nami nikauliza: Kuna mutu anayekuwa na hekima apate kueleza mambo haya? Ni nani aliyeongea na Yawe hata aweze kutangaza kwa nini inchi imeharibiwa na kufanywa tupu kama jangwa hata hakuna mutu anayepita humo?


Ni kwa sababu ya zambi za manabii wake na makosa ya makuhani wake, ambao walimwanga damu ya watu wa haki katika muji wake.


Ninyi munawachukia wanaotetea haki na wenye kusema ukweli katika tribinali.


Usituhubirie sisi. Mambo kama hayo si ya kuhubiriwa. Sisi hatutapatwa na hasara!


Yesu akaingia ndani ya hekalu. Alipokuwa akifundisha, wakubwa wa makuhani pamoja na wasimamizi wa watu wakamufikia na kumwuliza: “Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Ni nani aliyekupa mamlaka yale?”


Lakini wakubwa wa makuhani na wasimamizi wa watu wakawashawishi wale waliokusanyika kwamba waombe Baraba afunguliwe, naye Yesu auawe.


Lakini wakubwa wa makuhani wakawachochea watu wamwombe Pilato awafungulie Baraba.


Yesu alisema maneno haya wakati alipokuwa akifundisha katika hekalu, kwenye sanduku za kuwekea matoleo. Hakuna mutu aliyemufunga, kwa sababu wakati wake ulikuwa haujatimia.


Kwa ajili ya hii, wakaokota mawe kwa kumutupia. Lakini Yesu akajificha na kutoka ndani ya hekalu.


Lakini Wayuda wakawashawishi wakubwa wa muji pamoja na wanawake wamoja wenye heshima, walioabudu Mungu. Wakawatesa Paulo na Barnaba hata wakawafukuza toka katika inchi yao.


Muji wote ukajaa fujo na watu wakakusanyika pale mbiombio. Wakamukamata Paulo na kumukokotea mpaka inje ya hekalu, na mara moja wakafunga milango yake.


Makutano walimusikiliza Paulo mpaka aliposema maneno yale. Kisha wakasema kwa nguvu: “Mumuteketeze mutu huyu! Mumwue, kwa maana hastahili kuishi!”


Mutu huyo hakutaka kuachana na Petro na Yoane. Kwa hiyo watu wote wakashangaa sana na kukimbilia kwenye baraza la hekalu wanaloita La Solomono.


Mitume walifanya maajabu na vitambulisho vingi katikati ya watu. Waamini wote walizoea kukusanyika katika Baraza wanaloliita La Solomono.


akiwaambia: “Tuliwakataza kwa nguvu musifundishe tena kwa jina la mutu huyu. Na sasa mumeeneza mafundisho yenu katika Yerusalema yote, nanyi munataka kutubebesha lazima ya kifo chake.”


Kwa maana tumemusikia akisema kwamba huyu Yesu wa Nazareti ataharibu hekalu hili na kugeuza desturi tulizopokea toka kwa Musa.”


Nyuma ya kuishinda ile inchi, Waisraeli wote pamoja wakakusanyika kule Shilo na kulisimika hema la kusanyiko.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ