Lakini wewe au watoto wako mukigeuka na kuacha kunifuata, musiposhika amri zangu na masharti niliyowapa, mukienda kutumikia miungu mingine na kuiabudu,
Lakini musiponisikiliza na mukiacha kuihesabu siku ya Sabato kama siku takatifu, musipoacha kubeba mizigo na kuingia nayo kupitia milango ya Yerusalema siku ya Sabato, basi nitawakisha moto katika milango yake, nao utateketeza nyumba zote nzuri za Yerusalema, wala hautazimika. –Ni ujumbe wa Yawe.
Nao walifika, wakaitwaa na kuirizi. Lakini wao hawakukusikiliza, wala hawakufuata sheria zako. Hawakutenda mambo uliyoamuru. Ndiyo maana utawafanya wapatwe na hasara hii.
Hasara hizi zimewapata mpaka leo kwa sababu muliitolea miungu mingine sadaka za kuteketezwa na kumukosea Yawe, mukakataa kusikiliza sauti yake au kufuata sheria yake, masharti yake na maagizo yake.
Kwa hiyo, kama vile nilivyoutendea muji wa Shilo, ndivyo nitakavyolitendea hekalu hili linalojulikana kwa jina langu, hekalu ambalo ninyi munalitegemea; ndiyo pahali hapa ambapo niliwapa ninyi na babu zenu.
Nitakapowapeleka katika inchi inayotiririka maziwa na asali, kama vile nilivyowaapia babu zao, nao watakula, watashiba na kunenepa, halafu watageukia miungu mingine na kuitumikia. Watanizarau na kuvunja agano langu.
Basi kuna mambo mawili, ahadi na kiapo, yasiyoweza kubadilika, na kuelekea hayo, Mungu hawezi kusema uongo. Kwa hivi, sisi tuliomukimbilia tunatiwa moyo sana na kushika kwa nguvu tumaini tulilowekewa.