Basi, Yawe akaniuliza: Yeremia! Unaona nini? Mimi nikamujibu: Ninaona tini. Zile nzuri ni nzuri sana, na zile mbaya ni mbaya sana hata hazifai kukuliwa.
Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Kama tini hizi zinavyokuwa nzuri, ndivyo nitakavyowaona kuwa wema watu wa Yuda ambao niliowaondoa toka nafasi hii na kuwapeleka katika uhamisho katika inchi ya Wababeli.