Na nyumba hii itaharibiwa na kuwa mabomoko. Kila mutu atakayepita karibu atashituka na kutikisa kichwa, na kuuliza: ‘Kwa nini Yawe amefanya hivyo kwa inchi hii na kwa nyumba hii?’
Kwa sababu wameniacha na kufukizia miungu mingine ubani kusudi watu wanikasirikishe kwa kazi zote za mikono yao, basi, kasirani yangu juu ya Yerusalema itawaka na haitaweza kutulizwa.
Kwa sababu wameniacha mimi na kufukizia miungu mingine ubani kusudi wanikasirikishe sana kwa kazi zote za mikono yao, basi kasirani yangu itamwagika juu ya pahali hapa wala haitatulizwa.
Wameurudilia uovu wa babu zao ambao walikataa kusikiliza maneno yangu; wanaiabudu miungu mingine na kuitumikia. Watu wa Israeli na watu wa Yuda wamevunja agano nililofanya na babu zao.
Watu wote waliowakuta waliwaua, na waadui zao wamesema: Sisi hatuna kosa, maana hao wamemukosea Yawe anayekuwa makao yao ya kweli; Yawe ambaye ni tegemeo la babu zao!
Lakini nitawaacha wachache waepuke vita, njaa na ugonjwa mukali; kusudi hao waweze kuwaelezea watu wa mataifa wanamoishi jinsi walivyotenda mabaya. Halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.
Mataifa yatajua kwamba Waisraeli walikwenda katika uhamisho kutokana na makosa yao wenyewe waliyonikosea. Waliniasi, nami nikageuka wasipate kuniona, nikawatoa katika mikono ya waadui zao wakauawa.
Utakuwa kitu cha kuzarauliwa na cha haya, mufano wa kitu cha kuchukiza kwa makabila yanayokuzunguka, wakati nitakapotimiza hukumu zangu juu yako kwa hasira na kasirani yangu kali. Ni mimi Yawe ninayasema hivyo.