Yeremia 22:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
2 Wewe mufalme wa Yuda unayetawala kwa kiti cha kifalme cha Daudi pamoja na wakubwa wa serikali yako na watu wako wanaopita katika milango hii, musikilize neno la Yawe.
Kisha Mikaya akasema: “Sasa sikia neno la Yawe: Nilimwona Yawe akiikaa katika kiti chake cha kifalme, na jeshi lote la mbinguni likisimama pembeni yake, upande wake wa kuume na wa kushoto.
Utasema hivi: Musikilize neno la Yawe, enyi wafalme wa Yuda nanyi wakaaji wa Yerusalema. Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Kweli ninaleta hasara kwenye nafasi hii, hata kila mumoja atakayesikia habari ile, atastajabu.
Kama mukishika neno hili nililowaambia, basi wafalme watakaotawala kwa kiti cha kifalme cha Daudi wataendelea kuingia wakipitia milango ya nyumba hii ya kifalme. Watapita pamoja na wakubwa wa serikali yao na watu wao, wakipanda juu ya farasi na magari yenye kukokotwa na farasi.
Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Kwenda usemezane na Zedekia, mufalme wa Yuda. Umwambie kwamba mimi Yawe ninasema hivi: Nimeutia muji huu katika mikono ya mufalme wa Babeli, naye atauteketeza kwa moto.
Basi, Yawe anasema hivi juu yake yeye Yoyakimu mufalme wa Yuda: Yeye hatakuwa na mutu wa uzao wake atakayeikalia kiti cha kifalme cha Daudi, na maiti yake itatupwa inje kwenye joto muchana na baridi kali usiku.