Tafazali, utuombee kwa Yawe, maana Nebukadneza mufalme wa Babeli anaanza kupigana vita nasi. Labda Yawe atatufanyia mumoja wa miujiza yake na kumurudisha Nebukadneza aache kutushambulia.
Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Zedekia, nitakugeuzia wewe mwenyewe silaha unazozitumia kwa kupigana na mufalme wa Babeli na waaskari wake wanaozunguka inje ya kuta za muji wenu. Nitazikusanya silaha zile katikati ya muji huu.
Maana Zedekia, mufalme wa Yuda, alikuwa amemufunga Yeremia akisema: Kwa nini unatabiri na kusema: Yawe anasema hivi: Mimi ninautia muji huu katika mikono ya mufalme wa Babeli, naye atauteka.