Angalia sasa. Unategemea Misri, utete uliovunjika ambao utamuchoma mukono mutu yeyote atakayeutegemea. Hivi ndivyo mufalme wa Misri anavyokuwa kwa wote wale wanaomutegemea.
Kusudi asiendelee kutawala akiwa kule Yerusalema, Neko mufalme wa Misri alimufunga kule Ribla katika inchi ya Hamati, akawalipisha watu wa Yuda kodi ya kilo elfu tatu na mia ine za feza na kilo makumi tatu na ine za zahabu.
Tumekuasi na kukukana, ee Yawe, tumekataa kukufuata, ewe Mungu wetu. Tunasema maneno ya kutesa na uasi, katika mioyo yetu tunatunga na kutoa maneno ya uongo.
Tangaza katika inchi ya Misri, uijulishe huko Migidoli, uijulishe huko Nofi na Tapanesi. Uwaambie: Mukae tayari kabisa maana upanga utawaangamiza kila nafasi.
Wakimbizi wanaochoka wanasimama chini ya kivuli cha Hesiboni. Moto umewaka huko katika muji; ulimi wa moto toka nyumba ya kifalme ya Sihoni; umeteketeza mipaka ya Moabu, umeunguza milima ya hao wanaopiga kelele.
Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitaharibu sanamu za miungu, na kukomesha miungu ya uongo ya muji wa Nofi. Hakutakuwa mukubwa tena huko Misri. Nitasababisha hofu itawale katika inchi ya Misri.