Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 18:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Na wakati chombo alichokitengeneza kilipoharibika katika mikono yake, yeye alifinyanga upya chombo kingine kwa kadiri ilivyomupendeza.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 18:4
5 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ole kwake mutu anayebishana na Muumba wake: chombo cha udongo kubishana na mufinyanzi wake! Udongo unamwuliza anayeufinyanga: Unatengeneza nini hapa? au kumwambia: Kazi yako si kamili!


Basi, nikatelemuka mpaka kwenye nyumba ya mufinyanzi, nikamukuta mufinyanzi akifanya kazi yake kwenye gurudumu la kufinyangia udongo.


Kisha neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:


Enyi Waisraeli! Mimi siwezi kuwafanya ninyi kama mufinyanzi huyu anavyofanya? –Ni ujumbe wa Yawe.– Mujue kwamba kama vile udongo unavyokuwa katika mikono ya mufinyanzi, ndivyo ninyi munavyokuwa katika mikono yangu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ