Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 17:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Moyo wa mutu ni mudanganyifu kuliko vitu vyote; hauwezi kuponyeshwa, hakuna anayeweza kuuelewa!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 17:9
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe alipoona uwingi wa uovu wa watu katika dunia, na kwamba kila kitu mwanadamu anachokusudia ndani ya moyo wake ni kiovu siku zote,


Harufu nzuri ya sadaka hiyo ikamupendeza Yawe, naye akasema ndani ya moyo wake: “Sitailaani tena inchi hata kidogo kwa sababu ya mwanadamu. Ninajua kwamba mawazo yake ni maovu tangu utoto wake. Wala sitaangamiza tena viumbe vyote kama vile nilivyofanya.


Katika barua hiyo Daudi aliandika hivi: “Umuweke Uria kwenye mustari wa mbele, pahali ambako mapigano ni makali kabisa, kisha umwache kule na kurudia nyuma kusudi apigwe, na akufe.”


Ninaitikia kabisa makosa yangu, siku zote ninaona waziwazi zambi yangu.


Wanafanya shauri baya wakijisemesha: “Tumetimiza sasa mipango yetu! Nani anayeweza kugundua mafikiri ya ndani ya mutu?”


Anayetegemea akili yake mwenyewe ni mupumbafu; lakini anayeishi kwa hekima atakuwa salama.


Hili ni jambo baya zaidi kati ya yote yanayotukia hapa chini ya jua, kwamba mwisho uleule unawapata wote. Tena, wakati wote wa maisha yao, wanadamu wanajaa uovu na wazimu, na kisha wanakufa.


Niwapige wapi tena, ninyi munaoendelea kuasi? Kichwa chote kinajaa vidonda, na moyo unaumia kabisa!


Tokea kwenye muguu mpaka kwenye kichwa hakuna chenye kuwa kizima; ni machubuko, alama za mapigo na vidonda vinavyovuja damu, vilivyokosa kusafishwa, kufungwa wala kutulizwa kwa mafuta.


Kisha akaniambia: Ufanye akili za watu hawa kuwa ngumu, masikio yao yasisikie, macho yao yasione; wasipate kuona kwa macho yao, wasipate kusikia kwa masikio yao, wasipate kuelewa kwa akili zao, na kunigeukia, nao wapate kupona.


Ninyi mumefanya vibaya zaidi kuliko babu zenu, maana kila mumoja wenu ni mwenye moyo mugumu na mwenye nia mbaya, wala hamunisikilizi.


Lakini wao hawakunitii wala kunitegea sikio. Lakini wakafuata mashauri yao wenyewe na ugumu wa mioyo yao, wakarudi nyuma pahali pa kusonga mbele.


Maana mioyo ya watu hawa imegeuka migumu, wameziba masikio yao, nao wamefunga macho yao, kusudi wasipate kuona, nao wasipate kusikia, wala wasipate kunigeukia, nami ningewaponyesha.’


Kwa maana ndani ya moyo munatoka mawazo mabaya yanayoleta uuaji, uzinzi, uasherati, wizi, ushuhuda wa uongo na matukano.


Yesu alisikia vile walivyosema, na kwa hiyo akawaambia: “Wenye afya nzuri hawahitaji muganga, ni wale wanaokuwa wagonjwa tu. Sikukuja kuwaita wenye haki kunifuata, lakini watenda mabaya.”


Ijapokuwa wanamujua Mungu, hawamutukuzi wala kumushukuru kama vile anavyostahili. Lakini mawazo yao yaligeukia mambo ya ovyo ovyo, na mioyo yao isiyokuwa na ufahamu ilibaki katika giza.


Maana kutokana na amri ile, zambi ilipata njia ya kunidanganya na kuniua kufuatana na amri ile ile.


Basi munapaswa kutupilia mbali ile hali yenu ya zamani, ule utu wenu wa zamani unaopotoka kufuatana na tamaa zake za udanganyifu.


Basi wandugu zangu, muangalie vizuri, kati yenu kusikuwe mutu mumoja mwenye moyo mubaya wa kutokuamini, aliyefikia hata kujitenga mbali na Mungu Mwenye Uzima.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ