Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 17:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Itawabidi kuiacha hiyo inchi yenu niliyowapa, nami nitawafanya muwatumikie waadui zenu katika inchi musiyoijua, kwa sababu hasira yangu imewaka kama moto usiozimika hata milele.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 17:4
34 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

basi, nitawahamisha watu wangu, Waisraeli, kutoka inchi hii ambayo nimewapa; vilevile na nyumba hii ambayo niliyoitakasa kwa ajili ya jina langu, nitaitupilia mbali nami, na kuifanya kitu cha kuchekelewa na kuzarauliwa kati ya watu wa mataifa yote.


Mufalme Nebukadneza wa Babeli akawapiga na kuwaua watu hao kule Ribla katika inchi ya Hamati. Hivyo watu wa Yuda wakapelekwa kuwa watumwa inje ya inchi yao.


Lakini amani ilipopatikana wakatenda zambi tena mbele yako, nawe ukawaacha watiwe katika mikono ya waadui zao wawatawale. Hata hivyo, walipotubu na kukulilia ukawasikiliza kutoka mbinguni. Na kwa kulingana na rehema zako nyingi, ukawaokoa mara nyingi.


Ewe Israeli, wakati Yawe atakapokufariji nyuma ya mateso, mahangaiko na utumwa uliofanyiwa,


Kweli, pahali pa kumuteketeza mufalme wa Asuria pamekwisha kutayarishwa muda murefu uliopita. Pahali penyewe ni shimo kubwa na pana. Kuna moto na kuni kwa uwingi. Yawe ataupulizia pumzi yake kama kijito cha kiberiti na kuuwasha.


Kwa hiyo hasira ya Yawe iliwawakia watu wake, akaunyoosha mukono wake juu yao, akawaazibu. Milima ikatetemeka, maiti zao zikakuwa kama takataka katika barabara za muji. Hata hivyo, hasira yake haijatulia, angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.


Lakini ninyi munaowasha moto, na kujifanyia silaha za mienge, mutembee kwa mwangaza wa moto huo, ndimi za moto muliowasha ninyi wenyewe. Kitu mutakachopata kutoka kwa Yawe ni hiki: ninyi mutalala chini na mateso makali.


Kisha watakwenda kuziona maiti za wale walioniasi. Wadudu watakaowakula hawatakufa, na moto utakaowachoma hautazimika hata kidogo. Watakuwa chukizo kwa watu wote.


Yawe anasema hivi: Nimeiacha nyumba yangu; nimeitupa mali yangu mimi mwenyewe. Israeli, mupenzi wangu wa moyo, nimemutoa katika mikono ya waadui zake.


Nitawafanya muwatumikie waadui zenu katika inchi musiyoijua kwa sababu hasira yangu imewaka kama moto usiozimika hata milele.


Kwa hiyo, nitawafukuza toka katika inchi hii na kuwapeleka mpaka kwenye inchi ambayo ninyi wenyewe wala babu zenu hawakuijua. Kule mutaitumikia miungu mingine usiku na muchana, wala sitawasikilia ninyi huruma. –Ni ujumbe wa Yawe.


Lakini wewe, ee Yawe, unajua mashauri yao ya kuniua. Usiwasamehe uovu wao, wala kufuta zambi zao. Waanguke chini mbele yako; uwapige wakati wa hasira yako.


Israeli ni mutumwa, au amezaliwa mutumwa? Hapana! Kwa nini basi amekuwa kama nyama anayewindwa?


Enyi jamaa ya Daudi, Yawe anasema hivi: Kila asubui muamue maneno kufuatana na sheria yangu, muwakomboe wote walionyanganywa mali zao toka katika mikono ya watesaji. Kama si vile, hasira yangu itawaka kama moto, wala hakuna atakayeweza kuizimisha, kwa sababu ya matendo yenu maovu.


Mbona huyu mutu Konia, amekuwa kama chungu kilichovunjika, ambacho kinazarauliwa na kutupwa inje? Kwa nini yeye na watoto wake wamefukuzwa, wametupwa katika inchi wasiyoijua?


Na watu wenu watakapouliza: Kwa nini Yawe, Mungu wetu, ametutendea mambo hayo yote? Wewe Yeremia utawajibu hivi: Ninyi mulimwacha Yawe, mukaitumikia miungu ya kigeni katika inchi yenu. Basi ndivyo mutakavyowatumikia watu wengine katika inchi isiyokuwa yenu.


Mimi sitawaazibu kwa ajili ya mambo haya? Nitaachilia taifa hili bila kulilipiza kisasi? –Ni ujumbe wa Yawe.


Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitaimwanga hasira yangu juu ya pahali hapa, juu ya wanadamu na nyama, miti katika mashamba na juu ya mazao ya inchi. Nayo nafasi hii itawaka moto wala hautaweza kuzimishwa.


Enyi wapita njia wote, hivi hamujali kitu? Muangalie, muone kama kuna aliyepatwa na uchungu kama mimi, uchungu Yawe alioniletea siku ya hasira yake kali.


Inchi yetu imepewa kwa wageni, nyumba zetu kwa watu wengine.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: tosha kitambulisho chako cha kifalme na taji yako, maana mambo hayatabaki kama yalivyokuwa. Wanaokuwa chini watanyanyuliwa, wanaokuwa juu watashushwa!


Nitaleta watu wa mataifa mabaya sana nao watarizi nyumba zao. Nitakikomesha kiburi chao, na pahali pao pa kutambikia patachafuliwa.


“Yawe atawafanya mushindwe na waadui zenu. Ninyi mutakwenda kuwashambulia kwa njia moja, lakini mutawakimbia kwa njia saba. Nanyi mutakuwa kinyaa kwa watu wote katika dunia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ