Basi, watu wakaacha kuabudu katika nyumba ya Yawe, Mungu wa babu zao, wakaanza kuabudu Maashera na sanamu. Kasirani ya Mungu ikawaka juu ya Yuda na Yerusalema kwa sababu ya kosa lile.
Maombi yake na jinsi Mungu alivyomupokea, zambi zake zote na ukosefu wa uaminifu kwake, pahali alipojenga pa kutambikia na jinsi alivyotengeneza sanamu za Ashera na sanamu zingine mbele ya kujinyenyekeza, vimeandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Waonaji.
Kwa maana alijenga tena pahali pa kuabudia miungu mingine palipokuwa pamebomolewa na baba yake Hezekia; akajenga mazabahu za kuabudia Mabali, na kutengeneza sanamu za Ashera. Vilevile, aliabudu jeshi la mbinguni na kulitumikia.
Hawataelekea tena mazabahu ambazo ni kazi za vidole vyao wenyewe, wala kuzitazamia tena kazi za mikono yao wenyewe, ni kusema sanamu za mungu Ashera na mazabahu za kufukizia ubani.
Yawe anasema: Tangu zamani wewe ulivunja nira yako, ulikata minyororo yako, ukasema: “Sitakutumikia”. Juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila muti wa majani mabichi, ukalala machali kama kahaba.
Katika siku ya utawala wa mufalme Yosia, Yawe aliniambia hivi: Umeona jinsi yule Israeli asiyekuwa mwaminifu alivyofanya? Aliniacha, akapanda juu ya kila kilima kirefu na kwenda chini ya kila muti wenye majani mabichi, akafanya ukahaba wake kule!
Watoto wanaokota kuni, wababa wanawakisha moto na wamama wanaponda unga kwa ajili ya kutengeneza mikate ya kumutambikia mungu wa kike, wanayemwita malkia wa mbinguni. Tena wananikasirikisha kwa kuitolea miungu mingine sadaka ya divai.
Maana nilipowapeleka katika ile inchi niliyoapa kuwapa, kila mara walipoona kilima kirefu au miti ya majani mengi, walianza kutoa matambiko na sadaka zao na kunichokoza. Kulekule walitoa sadaka za harufu nzuri na kutoa sadaka za kinywaji.