Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 15:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Na kama wakikuuliza: Tutaenda wapi? Wewe utawajibu kwamba: Yawe anasema hivi: Walioandikiwa kufa kwa ugonjwa mukali, watakufa kwa ugonjwa mukali, walioandikiwa kufa kwa vita, watakufa kwa vita, walioandikwa kufa kwa njaa, watakufa kwa njaa; nao walioandikiwa kupelekwa katika utumwa, watapelekwa katika utumwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 15:2
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Atakapofika ataiangamiza inchi ya Misri. Kwa hiyo waliopangiwa kufa kwa ugonjwa watakufa kwa ugonjwa, waliopangiwa kukamatwa mateka, watakamatwa mateka; waliopangiwa kufa kwa vita watakufia katika vita.


Basi, nikawaambia: “Sitakuwa muchungaji wenu tena. Atakayekufa akufe! Atakayeangamia aangamie! Na wale watakaobaki wakulane wao kwa wao.”


Mutu yule aliyekusudiwa kuwa mufungwa, atafungwa; na yule aliyekusudiwa kuuawa kwa upanga, atauawa kwa upanga. Kwa sababu hiyo, watu wa Mungu wanapaswa kuwa wavumilivu na wenye imani.”


Kisha kutimia kwa wakati wa kushambuliwa kwa muji wa Yerusalema, utachoma sehemu moja ya tatu ya nywele zako katikati ya muji. Sehemu ingine moja ya tatu utaikatakata kwa upanga ukiuzunguka muji. Sehemu ya tatu ya mwisho utaipeperusha kwa upepo, nami nitauchomoa upanga wangu na kuwafuatilia nyuma.


Sehemu moja ya tatu ya watu wako, ee Yerusalema, itakufa kwa ugonjwa mukali na kwa njaa. Sehemu ingine moja ya tatu itakufa katika vita. Na sehemu moja ya tatu inayobaki nitaisambaza pande zote za dunia na nitachomoa upanga wangu na kuwafuatilia nyuma.


Hata wakifunga, sitayasikiliza maombi yao, na hata wakinitolea sadaka za kuteketeza kwa moto na sadaka zingine, mimi sitazikubali. Lakini nitawaangamiza kwa vita, njaa na ugonjwa mukali.


Mutu atakayekimbia sauti ya woga atatumbukia ndani ya shimo; na mutu atakayetoka ndani ya shimo atanaswa katika mutego. Madirisha ya mbinguni yamefunguliwa, misingi ya dunia inatikisika.


Mambo yatakuwa kama mutu aliyekimbia simba, halafu anakutana na dubu! Au kama mutu anayerudi kwa nyumba yake, na kutia mukono wake kwenye ukuta, na kuumwa na nyoka.


Umetimiza yale uliyosema utatutendea sisi pamoja na watawala wetu kwa kuuazibu Yerusalema vikali zaidi ya muji mwingine wowote katika dunia.


Lakini Bwana wetu Yawe anasema: Tena nitauazibu Yerusalema kwa mapigo yangu mane ya hukumu kali: vita, njaa, nyama wakali na ugonjwa mukali, nipate kuangamiza watu na nyama ndani yake!


Na hao ambao waliowatabiria mambo hayo, maiti zao zitatupwa katika barabara za Yerusalema wakiuawa kwa njaa na vita, wala hakutakuwa mutu wa kuwazika wao wenyewe, wake zao, wabinti zao na wana wao. Mimi nitawabebesha lazima ya uovu wao wenyewe.


Hao watakufa kwa magonjwa makali, na hakuna atakayeomboleza juu yao wala kuwazika. Maiti zao zitabaki kama vile mboleo juu ya udongo. Wataangamia kwa vita na kwa njaa; na maiti zao zitakuwa chakula cha ndege na nyama wa pori.


Vilevile kwa nafasi hii nitaivuruga mipango ya watu wa Yuda na ya watu wa Yerusalema. Nitawatoa washindwe na kuuawa kwa panga na waadui zao, wale wanaovizia maisha yao. Nazo maiti zao nitaziacha kuwa chakula cha ndege na nyama wa pori.


Uwaambie kwamba wewe ni kitambulisho kwao; kama ulivyofanya ndivyo itakavyotendeka kwao: watakwenda katika uhamisho; watakamatwa mateka.


Uwaambie hivi: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kama vile ninavyoishi, hao wanaokaa katika miji hiyo inayokuwa mabomoko, wataagamia kwa upanga; anayekuwa katika vijiji nitamutoa akuliwe na nyama wakali; na wale wanaokuwa kwa milima na ndani ya mapango watakufa kwa ugonjwa mukali.


Hakuna! Mutajikunja tu kati ya wafungwa na kuangamia pamoja na wanaouawa katika vita. Hata hivyo, hasira yake haijatulia, angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ