Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 13:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Yawe anasema hivi: Hivi ndivyo nitakavyokiharibu kiburi cha watu Yuda na kiburi kikubwa cha watu wa Yerusalema.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 13:9
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kiburi kinatangulia maangamizi; majivuno yanatangulia maanguko.


Watu wa Yuda wanasema hivi: Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu, tunajua jinsi alivyojivuna sana; tumesikia juu ya majivuno, kiburi na mazarau yake; lakini majivuno yake hayo ni bure.


Ni Yawe wa majeshi! Yeye ndiye aliyeyapanga haya yote. Alifanya hivyo akiharibu kiburi chao na kuwapatisha haya waheshimiwa wake.


Kwanza nikakunywesha wakaaji wa Yerusalema na miji mingine ya Yuda, wafalme wake na wakubwa wa serikali yake kusudi ikuwe jangwa, ukiwa, kitu cha kuzomewa na cha kulaaniwa, kama inavyokuwa mpaka leo. Halafu nikakunywesha:


Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu; Moabu ana majivuno sana. Tumesikia juu ya kujiona, kiburi na majivuno yake; tumesikia jinsi anavyojisifu ndani ya moyo.


Walijivuna, wakafanya machukizo mbele yangu. Kwa hiyo niliwaangamiza mara tu nilipoyaona hayo.


Kwa majivuno yako ulimuzarau dada yako Sodoma.


Kiburi chenu nitakivunja kabisa kwa kufanya mbingu kule juu kuwa ngumu kama chuma na inchi yenu bila mvua ikuwe ngumu kama shaba.


Mwangamizaji amekuja kukushambulia, ee Ninawe. Chunga kuta zako! Weka ulinzi katika barabara! Ujiweke tayari! Kusanya nguvu zako zote!


Siku hiyo, hautapata haya kutokana na matendo yako ya kuniasi, maana nitawaondoa kati yako wale wanaojivuna na kujitukuza, nawe hautakuwa na kiburi tena kwenye mulima wangu mutakatifu.


Yesu akaongeza kusema: “Ninawaambia kwamba mutu huyu alirudia kwake akiwa amehesabiwa kuwa na haki mbele ya Mungu, lakini si yule Mufarisayo. Kwa maana kila mutu anayejiinua atashushwa, lakini anayejishusha atainuliwa.”


Lakini Mungu ametujalia neema kubwa zaidi, kwa maana Maandiko yanasema: “Mungu anapingana na wenye kiburi, lakini anawajalia wanyenyekevu neema.”


Na hivi vilevile, ninyi vijana, munapaswa kuwatii hao wazee. Ninyi wote munapaswa kuwa na unyenyekevu, mupate kutumikiana; maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mungu anawapinga wenye kiburi, lakini anawajalia wanyenyekevu neema.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ