Watu wa Yuda wanasema hivi: Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu, tunajua jinsi alivyojivuna sana; tumesikia juu ya majivuno, kiburi na mazarau yake; lakini majivuno yake hayo ni bure.
Kwanza nikakunywesha wakaaji wa Yerusalema na miji mingine ya Yuda, wafalme wake na wakubwa wa serikali yake kusudi ikuwe jangwa, ukiwa, kitu cha kuzomewa na cha kulaaniwa, kama inavyokuwa mpaka leo. Halafu nikakunywesha:
Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu; Moabu ana majivuno sana. Tumesikia juu ya kujiona, kiburi na majivuno yake; tumesikia jinsi anavyojisifu ndani ya moyo.
Siku hiyo, hautapata haya kutokana na matendo yako ya kuniasi, maana nitawaondoa kati yako wale wanaojivuna na kujitukuza, nawe hautakuwa na kiburi tena kwenye mulima wangu mutakatifu.
Yesu akaongeza kusema: “Ninawaambia kwamba mutu huyu alirudia kwake akiwa amehesabiwa kuwa na haki mbele ya Mungu, lakini si yule Mufarisayo. Kwa maana kila mutu anayejiinua atashushwa, lakini anayejishusha atainuliwa.”
Na hivi vilevile, ninyi vijana, munapaswa kuwatii hao wazee. Ninyi wote munapaswa kuwa na unyenyekevu, mupate kutumikiana; maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mungu anawapinga wenye kiburi, lakini anawajalia wanyenyekevu neema.”