5 Basi, nikaenda na kuficha ule mukaba karibu na muto Furati, kama vile Yawe alivyoniamuru.
Basi, Musa alitimiza kwa ukamilifu kabisa maagizo yote ya Yawe.
Kulipokwisha kupita siku nyingi, Yawe akaniambia: Kwenda kwenye muto Furati, utwae ule mukaba niliokuamuru kuuficha huko.
Basi, nikatoa unabii kama nilivyoamriwa. Nilipokuwa nikitoa unabii, kukatokea kelele kama ya mukwaruzo na ile mifupa ikaanza kusogeleana na kuungana.
Ushiriki katika mateso kama vile askari mwema wa Kristo Yesu.
Kwa njia ya imani, Abrahamu alitii wakati Mungu alipomwita na kwenda katika inchi ile Mungu aliyoahidi kumupatia kuwa urizi wake. Akaacha inchi yake pasipo kujua pahali anapokwenda.