Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 11:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Hili ni agano nililowaagiza babu zenu kutii nilipowaondoa katika inchi ya Misri, kutoka katika shimo la moto. Niliwaambia wanitii na kufanya yote niliyowaamuru, na kwamba wakifanya hivyo, watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 11:4
39 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nitakupa wewe na wazao wako inchi hii ambamo unaishi kama mugeni. Ni kusema inchi yote ya Kanana ikuwe mali yenu milele; nami nitakuwa Mungu wao.”


maana ni watu wako, na ni mali yako, watu ambao uliwatoa Misri kutoka katika furu ya chuma.


Yeye hakumwasi Yawe wala hakuacha kumufuata, lakini alishika amri ambazo Yawe alimupa Musa.


Lakini ninawatendea mema maelfu ya wale wanaonipenda na kushika amri zangu.


Ujumbe wa Mungu juu ya nyama wa pande za jangwa ya kusini: Wajumbe wanapita katika inchi ya taabu na shida, yenye simba, nyoka wa sumu na nyoka wakubwa wanaoruka. Wamewabebesha punda na ngamia wao mali zao, kuwapelekea watu wasioweza kuwafalia kitu.


Mimi nimekusafisha lakini si kama feza katika furu. Nimewapima katika furu ya taabu.


Maana niliwaonya vikali babu zao nilipowaondoa katika inchi ya Misri, nami nimeendelea kuwaonya wanitii mpaka siku hii ya leo.


Nitawapa moyo wa kujua kwamba mimi ndimi Yawe. Watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao; maana watanirudilia kwa moyo wao wote.


Sasa basi, mugeuze mienendo yenu na matendo yenu na kutii sauti ya Yawe, Mungu wenu. Mukifanya hivyo, Yawe atabadilisha nia yake na kuacha kuwaletea hasara aliyokusudia kuleta juu yenu.


Mutakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu.


Yawe anasema hivi: Kwa hiyo, ninautoa muji huu kwa Wakaldea na kwa Nebukadneza mufalme wa Babeli, naye atauteka.


Yeremia akamujibu: Hautatolewa kwao. Wewe sasa utii kile Yawe anachosema, kama ninavyokuambia, na mambo yote yatakuendekea vema, na maisha yako yataokolewa.


kusudi mupate kufuata masharti yangu na kuyatii maagizo yangu; nanyi mutakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wenu.


Kwa hiyo Waisraeli hawataniacha tena na kujichafua wenyewe kwa kutenda zambi; kusudi wakuwe watu wangu nami nikuwe Mungu wao. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Mutakaa katika inchi niliyopatia wazee wenu. Mutakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu.


Hawatajichafua tena kwa kuabudu sanamu za miungu yao na kwa mambo yao ya kuchukiza wala kwa makosa yao. Nitawaokoa wasikuwe tena waasi. Nao watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao.


Nitaishi kati yao; nitakuwa Mungu wao nao watakuwa watu wangu.


Basi, mufalme Nebukadneza akaukaribia mulango wa furu la moto mukali, akaita: Sadiraki, Mesaki na Abedenego, watumishi wa Mungu Mukubwa, mutoke mukuje hapa! Sadiraki, Mesaki na Abedenego wakatoka ndani ya moto.


Nitatembea kati yenu na kuwa Mungu wenu nanyi mutakuwa watu wangu.


Kama mukifuata masharti yangu na kushika amri zangu,


Sehemu hiyo moja ya tatu itakayobaki, nitaipima na kuitakasa, kama vile mutu anavyosafisha feza, kama vile wanavyopima zahabu. Halafu wao wataniomba mimi, nami nitawajibu. Nitasema: Hawa ni watu wangu, nao watasema: Yawe, ndiye Mungu wetu.


Watu wanaokaa katika inchi za mbali watakuja kusaidia kwa kulijenga hekalu langu mimi Yawe. Nanyi mutajua kwamba Yawe wa majeshi, ndiye aliyenituma kwenu. Haya yote yatatukia kama mukiitii sauti ya Yawe, Mungu wenu.


na kuwafanya wakae katika Yerusalema. Wao watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao; nitatawala juu yao kwa uaminifu na haki.


Muwafundishe kutii maneno yote niliyowaagiza. Na mujue kwamba mimi ni pamoja nanyi siku zote hata mwisho wa dunia.”


Kuna ulinganisho gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa maana sisi ni hekalu la Mungu Mwenye Uzima kama vile yeye mwenyewe alivyosema: “Nitakaa na kuishi pamoja nao, nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”


baraka, kama mutatii amri za Yawe, Mungu wenu, ambazo ninawapa hivi leo;


Lakini ninyi ndio watu aliowakomboa kutoka Misri katika furu la chuma. Aliwatoa huko kusudi mukuwe watu wake kama vile munavyokuwa hivi leo.


“Mimi ni Yawe, Mungu wako, niliyekutoa katika inchi ya Misri, ambako ulikuwa mutumwa.


Na alipokwisha kufanywa kuwa mukamilifu, akawaongoza watu wote wanaomutii wapate kuokolewa kwa milele.


Halafu Samweli akamwambia: “Unazani kwamba Yawe anapendelea zaidi sadaka za kuteketezwa kwa moto na matoleo mengine, kuliko kuitii sauti yake? Hapana. Kumutii yeye ni bora kuliko matoleo na kumusikiliza kuliko kumutolea mafuta ya beberu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ