Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 10:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Sanamu hizo zinapambwa kwa feza kutoka Tarsisi, na zahabu kutoka Ofiri; zilitengenezwa na wafundi na wafua zahabu. Zimevalishwa nguo nzuri za rangi ya samawi na nyekundu-nyeusi, zilizofumwa na wafundi wa kufuma.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 10:9
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa sababu mufalme Solomono alikuwa na mashua kubwa za Tarsisi zilizokuwa zikisafiri pamoja na mashua za Hiramu, kisha kila miaka mitatu mashua hizo za Tarsisi zilimuletea mufalme zahabu, feza, pembe, kima, na tausi.


Solomono alikuwa na mashua zilizosafiri mpaka Tarsisi na watumishi wa Hiramu, na kisha kila miaka mitatu, mashua zile zilirudi zikimuletea zahabu, feza, pembe, kima na ndege wanaoitwa tausi.


Miungu yao ni ya feza na zahabu; imetengenezwa kwa mikono ya wanadamu.


Wafalme wa Tarsisi na visiwa wamulipe kodi, wafalme wa Sheba na Seba wamuletee zawadi.


Muomboleze enyi wenyeji wa Foinike! Mujaribu kukimbilia Tarsisi.


Anafanana na sanamu? Hiyo, fundi anaichonga, mufuaji wa zahabu anaipakaa zahabu, na kuitengenezea mukufu wa feza!


Watu wa Tarsisi walifanya biashara nawe kwa sababu ya utajiri wako mwingi na wa kila namna. Walitoa feza, chuma, bati, na risasi kwa kupata biashara yako.


Kitani kilichopindwa vizuri kutoka Misri kilikuwa kwa kupamba tanga lako na kwa ajili ya bendera yako. Chandarua chako kilitengenezwa na nguo ya rangi ya samawi na nyekundu-nyeusi kutoka visanga vya Elisa.


Nikainua macho, nikamwona mutu anayevaa nguo za kitani naye alikuwa amejifunga mukaba wa zahabu safi kutoka Ufasi.


Ile sanamu inatoka Israeli, ni fundi ndiye aliyeitengeneza. Yenyewe si Mungu hata kidogo. Kweli! Sanamu ya mwana-ngombe ya Samaria itavunjwavunjwa!


Basi, Yona akasimama kwa kukimbilia Tarsisi, mbali na uso wa Yawe. Akaenda mpaka katika muji wa Yofa ambapo alikuta mashua moja iko tayari kwenda Tarsisi. Alilipa bei ya safari, akapanda ndani ya mashua, akasafiri pamoja na watu wengine kwenda Tarsisi, mbali na uso wa Yawe.


Ole wake mutu anayeambia kipande cha muti: Amuka! au jiwe bubu: Simama! Sanamu inaweza kumufundisha mutu? Angalia imepakwa zahabu na feza, lakini haina uzima wowote.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ