Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 10:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Sanamu zao ni kama sanamu za kutishia ndege katika shamba la maboga, hazina uwezo wa kuongea; ni lazima zibebwe maana haziwezi kutembea. Musiziogope sanamu hizo, maana haziwezi kuzuru, wala haziwezi kutenda jambo lolote jema.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 10:5
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hao manabii wakamutwaa ngombe dume wao waliyepewa, wakamutayarisha, kisha wakaanza kumulilia Bali kutokea asubui mpaka saa sita za muchana, wakirukaruka pembeni ya mazabahu waliyotengeneza wakisema: “Ee Bali, utusikilize!” Lakini hakukutokea sauti yoyote, wala hakuna aliyewajibu.


Hayo yakamukasirisha sana Yawe, akatuma nabii kwa Amazia. Nabii huyo akamwuliza Amazia: “Kwa nini unategemea miungu ya watu wengine ambayo hata haikuweza kuwaokoa watu wake wenyewe kutoka katika mikono yako?”


Watu wa Moabu wanapojitokeza kuabudu mungu wao, wanapojichokesha huko juu pahali pa ibada, wanapokwenda pahali pao patakatifu kwa kuomba, hawatakubaliwa.


Enyi watu wa mataifa muliobaki, mukusanyike pamoja mukuje! Ninyi mumekosa akili: ninyi munabeba sanamu za miti na kumwomba mungu asiyeweza kuokoa watu.


Ule mungu Bali ameanguka; mungu Nebo anainama. Sanamu zao zinabebwa juu ya nyama, juu ya nyama wanaobeba mizigo! Vitu ninyi mulivyokuwa mukiviinua juu, vinakuwa sasa mizigo, vinakuwa mizigo mizito juu ya nyama wenye kuchoka.


Wanajibebesha sanamu hiyo juu ya mabega na kuipeleka, kisha wanaiweka pahali pake, nayo inakaa palepale; haiwezi hata kidogo kusogea kutoka pale inapokuwa. Mutu akiililia, haiwezi kumwitikia, wala haiwezi kumwokoa mutu katika taabu zake.


Mwanadamu ni mujinga na mupumbafu; kila mufua zahabu anafezeheshwa na sanamu zake. Sanamu hizo ni uongo mutupu, hazina uzima wowote ndani yao.


Ole wake mutu anayeambia kipande cha muti: Amuka! au jiwe bubu: Simama! Sanamu inaweza kumufundisha mutu? Angalia imepakwa zahabu na feza, lakini haina uzima wowote.


Munajua kwamba wakati mulipokuwa wapagani, mulikuwa mukivutwa na kupotoshwa na sanamu zisizosema.


Basi kuelekea lile ulizo juu ya kula nyama za kutambikiwa kwa sanamu za miungu, tunajua kwamba sanamu ni kitu bure katika dunia, na ya kuwa kuna Mungu mumoja peke yake tu.


Huko mutatumikia miungu ya miti na mawe ambayo imetengenezwa kwa mikono ya watu na ambayo haiwezi kuona, haisikii, haikuli wala kunusa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ