Mufuaji wa vyuma anatwaa kipande cha chuma, anakiyeyusha kwa moto na kufua sanamu. Anakipondaponda na nyundo kusudi akipatie umbo kwa mikono yake yenye nguvu. Wakati wote huo yeye anasikia njaa na kuchoka; anasikia kiu na nguvu kuregea.
Watu wanapoteza zahabu kutoka mifuko yao, wanapima feza kwenye mizani zao, wanamulipa mufuaji wa zahabu awatengenezee sanamu ya mungu, kisha wanainama mbele yake na kuiabudu!
Wanajibebesha sanamu hiyo juu ya mabega na kuipeleka, kisha wanaiweka pahali pake, nayo inakaa palepale; haiwezi hata kidogo kusogea kutoka pale inapokuwa. Mutu akiililia, haiwezi kumwitikia, wala haiwezi kumwokoa mutu katika taabu zake.
Waefuraimu wanaendelea kutenda zambi, wanajitengenezea sanamu za feza yenye kuyeyushwa, sanamu zinazotengenezwa kwa ufundi wao, zote zikiwa kazi ya wafundi. Wanasema: Muzitambikie! Wanaume wanabusu sanamu ya mwana-ngombe!
Ole wake mutu anayeambia kipande cha muti: Amuka! au jiwe bubu: Simama! Sanamu inaweza kumufundisha mutu? Angalia imepakwa zahabu na feza, lakini haina uzima wowote.