Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yeremia 10:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Enyi Waisraeli musikilize neno Yawe analowaambia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yeremia 10:1
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha Mikaya akasema: “Sasa sikia neno la Yawe: Nilimwona Yawe akiikaa katika kiti chake cha kifalme, na jeshi lote la mbinguni likisimama pembeni yake, upande wake wa kuume na wa kushoto.


“Enyi watu wangu, munisikilize, mimi Mungu, Mungu wenu! Ninataka kusema nanyi. Israeli, ninakuonya.


Musikilize neno la Yawe, enyi watawala waovu kama wa Sodoma! Musikilize mafundisho ya Mungu wetu, enyi watu waovu kama wa Gomora!


Basi, musikilize neno la Yawe, enyi wenye mazarau munaotawala watu wa Yerusalema:


Mutamulinganisha Mungu na nini basi, au ni kitu gani cha kumufananisha nacho?


Yawe, Mufalme na Mukombozi wa Israeli, Yawe wa majeshi anasema hivi: Mimi ni wa kwanza na wa mwisho; hakuna mungu mwingine isipokuwa mimi.


Yawe anasema hivi: Musiige mwenendo wa mataifa mengine, wala musishangazwe na vitambulisho vya ajabu munavyoviona katika mbingu; muyaache mataifa mengine yashangazwe navyo.


Musikilize neno la Yawe, enyi wazao wa Yakobo. Musikilize, enyi jamaa zote za wazao wa Israeli.


Wewe mufalme wa Yuda unayetawala kwa kiti cha kifalme cha Daudi pamoja na wakubwa wa serikali yako na watu wako wanaopita katika milango hii, musikilize neno la Yawe.


basi, musikilize jinsi Yawe anavyosema enyi mabaki ya Yuda. Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Kama mumekusudia kwenda katika inchi ya Misri na kukaa huko,


Musikilize maneno ya Yawe, enyi Waisraeli. Yawe anawashitaki wakaaji wa inchi hii. Hakuna tena uaminifu wala wema katika inchi; hakuna anayemujua Mungu katika inchi hii.


Nawe basi, ewe Amazia, sikiliza neno la Yawe: Wewe unaniambia nisitoe unabii juu ya Waisraeli, wala nisiseme neno lolote juu ya wazao wa Isaka.


Inatupasa tena kumushukuru Mungu siku zote kwa ajili ya jambo hili: muliposikia neno la Mungu kutoka kwetu, hamukulikubali kama vile neno la mutu, lakini kama vile kweli ndilo neno la Mungu. Na neno lile ndilo linalofanya kazi ndani ya mioyo yenu ninyi wanaoamini.


“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa!


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ